MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 19 December 2014

POLISI YAANZA MSAKO MKALI, MAUAJI YA KUTATANISHA MANISPAA BUKOBA,YAWASIHI WANANCHI KUONDOA KARANTINI YA KUJIFUNGIA KABLA YA MUDA WA USIKU.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe, amesema kuwa sasa wameanza doria kaliambayo inahusisha maeneo yote muhimu na yenye taarifa za mauaji,huku watu watatu wameshakamatwa kuhusiana na mauaji katika manispaa ya Bukoba.


Kamanda Mwaibambe, amekiri kuwapo kwa mauaji ya kutatanisha, alipoongea na mwandishi wa habari hii ya uchunguzi Nicolaus Mac Ngaiza, kuhusu mauaji ya kutatanisha manispaa ya Bukoba, huku akisema kuwa polisi haiwezi kuficha huku wananchi wakipoteza maisha na kuishi bila amani.

Amesema kuwa kutokana na rekodi za vifo kuanzia October 6 hadi December 5 2014, kama makala ya mwandishi inavyosema, wamepitia taarifa zao na kugundua kuna vifo vya watu saba vya kufanana ambavyo hatahivyo haviusiani na imani za kishirikina, kwani hakuna kiungo kinachoondolewa baada ya mtu kuuawa.

ACP Mwaibambe, amewataja waliouawa kuwa ni Mwl Ng’wandu, Mozes Kashaga, Ernest Kato, Goodrack Francis, Rutu, na vijana wawili ambao hawakutambulika, majina mmoja akikutwa kwenye shamba la mwananchi mmoja Kitendaguro,hukumwingine akikutwa kwenye Bwawa la maji kata Kashai,ilhaliakiwa na jeraha la kukatwa na kitu cha ncha kali kichwani.

Amewataka wananchi kuviamini vyombo vya dola, hukuakiongeza kuwa watakuwa wakiwajulisha wananchi kila kinachoendelea lakini akawaomba kusaidia jeshi hilo kufichua wahusika na kusema kuwa sasa wanazweza kuendelea shughuli zao za kibiashara tofauti na kujifungia saa za jioni kuhofia maisha yao.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: