Lengo
kuu la siku hizi 16 ni kuendeleza
mijadala, kutafakari kwa pamoja kuhusu
mikakati ya kutokomeza ukatili wa kijinsia, mafanikio yake, changamoto na namna
ya kujipanga na kusonga mbele kwa
pamoja. Kila mwaka kunakuwa na kauli
mbiu na kauli mbiu ya mwaka huu hapa Tanzania ni “Funguka!
Fichua Ukatili kwa afya ya jamii” Hii ina
maana kuwa tuvunje ukimya kila tunaposhuhudia kitendo chochote cha ukatili wa
kijinsia tuchukue hatua. Aidha
kauli mbiu itayoongoza mjadala wetu wa leo ni “Siyumbishi, Najilinda Mnilinde” kauli
mbiu hii inalenga vijana kwani tunaamini kuwa mapambano haya yanahitaji nguvu
kubwa na ya pamoja. Vijana ni zaidi ya
60% ya watanzania wote. Hii ni idadi kubwa sana.
Tunatarajia hawa vijana ndio
watakaoendesha taifa hili kwa miaka hamsini ijayo hivyo basi mikakati yetu lazima iwalenge
vijana. Vijana hususan vijana wa kike
wanakabiliwa pia na ukatili wa kijinsia
kwa kiasi kikubwa. Hivyo basi wanatakiwa kujilinda dhidi ya mazingira hararishi ambayo yanaweza
kuwasababishia kukumbana na ukatili wa kijinsia. Jamii pia inajukumu kubwa la la kuwalinda vijana katika kuwatayarishia mazingira bora dhidi ya ukatili wa kijinsia kuanzia nyumbani,
shuleni vyuni hadi maofisini.
Tatizo la jira ni kubwa sana
na kwa kiasi kikubwa linasababisha ukatili kwa wasichana hususan ule wa ajira zisizo na utu, usafirishaji
haramu wa wasichana, biashara ya ngono,
rushwa ya ngono , ndoa za utotoni n.k. Tunasisitiza uwepo wa mabweni ya kutosha katika shule zote za
sekondari za kata na nyigine hususan ya wasichana ili kupunguza umbali na mazingira hatarishi kwenda shuleni.
"Tunatarajia kuwa baada ya
mjadala huu vuijana wetu watakuwa mabalozi wa kupinga ukatili wa kijinsia na kuitekeleza
kauli mbiu hii ya kutokuyumbisha,
kujilinda na jamii kuwalinda".
Ndugu mgeni rasmi, TGNP kwa kushirikina na
wadau wengine tunaungana na wenzetu kote duniani kupinga ukatili wa kijinsia.
Mapambano haya yameanza muda mrefu japokuwa hali bado si nzuri kwani takwimu zinaonesha kwamba 1/3 ya wanawake waliona umri kati ya miaka 15 –
49 wamefanyiwa ukatili wa kijinsia na
wenzi au ndugu zao. Wanawake 2 kati ya 5
wamefanyiwa ukatili tangu wakiwa na miaka 15. Asilimia 44 ya wanawake walio katika ndoa kati ya umri wa
miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili na wenzi
wao. 20% ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa
ukatili wa kingono na wapenzi wao.
Takwimu za wizara ya afya zinaonesha, katika mwaka 2013
asilimia 23% ya wasichana wenye umri kati ya miaka 15 na 19 walikuwa na mimba
au walikuwa na watoto huku zikionesha kuwa asilimia 18% ya wasichana wa umri
huo huolewa utotoni. Wasichana 4 kati ya 10 ni wahanga wa mimba za
utotoni. Mwaka 2012 wasichana 8000
waliacha shule kutokana na mimba za utotoni na kati ya hao 3000 walikuwa shule
za msingi. Takwimu hizo pia zinaonesha kuwa bado ukeketaji ni tatizo kubwa
likiwa bado linatendeka kwa asilimia 15%.
Pia asilimia 14.6 ya
wanawake wa Tanzania wamefanyiwa ukeketaji. Mikoa inayoongoza kwa ukeketaji
ni manyara 70.8%, Arusha 58.6% na Mara 39.0% ( 2010).Hali hii inatisha na inahitaji
nguvu ya ziada ili kukomesha
ukatili huu.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment