MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 3 December 2014

NEWS ALERT!!! WAKATI KAGERA UCHAFUZI WA ZIWA VICTORIA, GEITA UCHAFUZI KUPITIA MIGODI WATAWALA

 Hali ya sasa ya maji kandokando mwa ziwa Victoria hasa eneo lamji wa Bukoba, yanatisha kwa uchafu huku yakiwa na ragi ya kijani na kujaa takataka kutokana na matumizi ya kibinadamu.

Maji hayo yanaweza kuhatarisha maisha ya watu kutokana na uchafu huo ambapo watoto upendelea kuogelea katikamaeneo kadhaa ya ziwa hilo.




UCHAFUZI wa mazingira kwa maeneo yanayozunguka shughuli za uchimbaji madini ukiwemo mgodi wa dhahabu wa Geita Gold Mine(GGM) hautaisha endapo jamii haitashirikishwa na wenye makampuni wanaoendesha shughuli za kimadini ambao pia ni vyanzo vya uchafuzi huo.

Aidha mji wa Geita unaozungukwa na shughuli za uchimbaji kumekuwepo na malalamiko mengi juu ya athari za kimazingira jambo ambalo watu mbalimbali wamekuwa wakifika kufanya tafiti tofauti ili kubaini madhara ya athari hizo zinazoongelewa kila mara katika jamii.

Mhadhiri wa chuo kikuu cha Mzumbe kitivo cha sheria Hanifa Massawe amekuwa miongoni mwa watafiti wa uharibifu wa mazingira katika mji wa Geita kutokana na shughuli za kimadini zinazoendelea kwa mda mrefu bila kuzipatia majawabu kwa jamii.

Baadhi ya sababu alizokutana nazo wakati wa tafiti hiyo ni pamoja na uchafuzi wa vyanzo vya maji yanayotumika,uchafuzi wa aridhi katika ulipuaji wa miamba kwa wachimbaji wakubwa na wadogo waliopo maeneo ya samina,Mponvu,mgusu na Nyakabale maeneo ambayo uchimbaji upo kwa wingi.

Hivyo mhadhiri huyo ameshauri kuwa changamoto hizi zitafutiwe majawabu na mamlaka husika kwa wakati kwani huenda hazitafutiwi ufumbuzi kutokana na mamlaka zinazohusika kutotilia mkazo mambo hayo lakini pia mamlaka hazifuatilii kwa karibu matatizo hayo.

Wakati huohuo katibu wa kituo cha sheria na haki za binadamu  wilaya ya Geita Elineema Mafie amesema kuwa hari ya mahusiano kati ya wachimbaji na wananchi hususani mgodi mkubwa wa GGM siyo ya kuridhisha kiasi kwamba ukuikwaji wa haki za binadamu unajitokeza sana na upo kwa mda mrefu bila kuupatia ufumbuzi wake.

Ameongeza kuwa kumekuwa na mahusiano kati ya mgodi na viongozi wa mitaa hususani wenyeviti wakiwa na vikao vya mahusiano lakini cha ajabu wenyeviti hao hawarudishi majibu kwa wananchi ambao ndio wahanga wa matukio hayo hivyo ametaka kuwepo utaratibu wa wenyeviti kukaa na wananchi ili kuwapa mrejesho juu ya mahusiani wanayofanya mgodi.

Na Mwanaharakati.

No comments: