MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 30 January 2015

HATARI KWA WAFANYAKAZI WA KITANZANIA VIWANDANI PWANI





Ni kutokana na baadhi ya wamiliki wa viwanda mkoani humo kukiuka sheria za usalama mahali pa kazi kwa kuwafanyisha kazi kinyume na taratibu.

Hali hiyo ya kuhofia kukamatwa imekuwa ikiwafanya kufunga Geit za viwanda vyao ili wakaguzi wa serikali wasiwafikie kama inavyoonekana katika kiwanda cha BLANKETS & TEKTILE cha Mkuranga, huku Tanzania Gyp sum waliofungua wamebainika kuwanyanyasa wafanyakazi kwa kuwanyima vitendea kazi huku wakifanyika katika eneo lenye hali mbaya ya hewa.

Kiwanda hicho kinajihusisha na utengenezaji wa GYPSUM ambazo hutumika kwenye ujenzi ambapo utengenezaji wake unahitaji vifaa kama boots, groves na vifaa vya kuvaa usoni, lakini wao wanakiuka kama picha moja inavyoonesha mfanyakazi akiendelea kuteseka kazini hapo juu, huku weneyewe wachina wakijifungia kwenye vibanda vidogo vya vioo wanavyotengeneza na kuwekea vioyozi ili waendelee kusimamia utendaji kazi.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: