![]() |
Godfrey Joseph Kajuna (45miaka) |

Ni Godfrey Joseph Kajuna (45miaka) alikuwa
mkaazi katika Kitongoji cha Buyumba,Kijiji cha Bushemba,Kata ya Buganguzi
Wilayani Muleba Mkoa wa Kagera amejinyonga hadi kufa baada ya kumfanyia ukatili
mtoto wake wa kuzaa.
Inasemekana kuwa baba huyo alimpiga
na kumjeruhi kichwani kwa fimbo nzito kisha akamtoboa macho, mwanae aitwaye Agripina Godfrey (12) anayesoma darasa
la Kwanza katika shule ya msingi Ilambika.
Taarifa za awali zisizo rasmi zinasema Baba alitoka ndani na kuwaambia wanae kuwa Mama yao akirudi wasimfungulie mlango, ndipo mama aliporudi watoto kwa kumuogopa Baba yao wakakataa kumfungulia Mlango.
Mama akaondoka kujiifadhi
sehemu.
Baba yao aliporudi akawauliza Mama yao yuko wapi,ndipo huyo mtoto aliyeonekana kama ndiyo mkubwa kwenye familia hiyo akamjibu Baba yake kuwa "Baba si ulisema mama akija tusimfungulie?" Hali hiyo ikamfanya Baba yake aanze kumpiga sana! Mpaka kumuumiza vile.
Damu zikaanza kumtoka mtoto,Baba mtoto akachukua Chumvi na kuanza kuimimina kwenye jeraha kichwani na alipoonekana kama hali inakuwa Mbaya… Baba akaandika kijibarua haraka na kusema kuwa kwa kitendo alichofanya na vitendo vingine ambavyo huwa anaifanyia familia hiyo ameogopa kukamatwa… akajitundika kwenye Kamba na kujimaliza yeye mwenyewe.
Baba yao aliporudi akawauliza Mama yao yuko wapi,ndipo huyo mtoto aliyeonekana kama ndiyo mkubwa kwenye familia hiyo akamjibu Baba yake kuwa "Baba si ulisema mama akija tusimfungulie?" Hali hiyo ikamfanya Baba yake aanze kumpiga sana! Mpaka kumuumiza vile.
Damu zikaanza kumtoka mtoto,Baba mtoto akachukua Chumvi na kuanza kuimimina kwenye jeraha kichwani na alipoonekana kama hali inakuwa Mbaya… Baba akaandika kijibarua haraka na kusema kuwa kwa kitendo alichofanya na vitendo vingine ambavyo huwa anaifanyia familia hiyo ameogopa kukamatwa… akajitundika kwenye Kamba na kujimaliza yeye mwenyewe.
Mtoto alipelekwa katika Hospitali
teule ya Wilaya ya Muleba (Rubya Hospital) kwa matibabu zaidi.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment