MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 14 January 2015

KIJANA AUAWA KWA UTATA GEITA



WAKAZI wa kijiji cha Nkome wilayani Geita, wameamua kutelekeza nje ya kituo cha polisi Nkome maiti ya kijana mmoja anayesadikiwa kupigwa na  baadhi ya watu.

Tetesi zinasema kuwa kifo hicho kimetokea ndani ya kituo hicho na kusababisha kifo chake.

Aliyeuawa ametambulika kuwa ni Mlangila Tigamanywa(22), mkazi wa mtaa wa Yakaranda,kijiji cha Nkome Tarafa ya Bugando wilayani hapa.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nkome Anjero Daniel,amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kwamba lilitokea Desemba 19 mwaka jana  majira ya usiku muda mfupi baada ya mzazi wa kijana huyo Bigamanywa Mlangila kumfikisha mwanaye huyo lkituoni hapo.

Akielezea tukio hilo,kaka wa marehemu,Galindi Lukanazya(35), aliliambia Tanzania Daima kuwa nduguye alipigwa na askari wawili wa kituo hicho aliowataja kwa majina ya PC Simon na mgambo wa kituo hicho Mashaka Desemba 19,2014.

Alisema,mdogo wake baada ya kufikishwa kituoni hapo na baba yake mzazi akiwa na afya njema majira ya jioni aliwekwa rockup na baadaye baba yake aliondoka kituoni hapo akitakiwa afike kesho yake kwa ajili ya kuchukuliwa maelezo.

Hata hivyo,majira ya saa 2 usiku wakati mkuu wa kituo hicho Gwaga Mtawa akiwa amekwenda kuangalia taarifa ya habari kwenye kumbi za starehe Mgambo na askari huyo walimtoa mdogo wake huyo Rockup na kuanza kumpiga hadi akazirai na kumrejesha tena rockup.

Kwa mjibu wa Lukanazya,baba wa marehemu alifikia hatua ya kumpeleka polisi mtoto wake huyo baada ya kuvunja dirisha la nyumba yao hali iliyomchukiza na kuamua kumfikisha kituo cha polisi.

‘’Ni kwamba,baba aliweka mpangaji kwenye chumba alichokuwa analala marehemu,marehemu akamuuliza baba yake kama anaweka mpangaji yeye atalala wapi na baba yake alimjibu atafute pa kulala kwani nyumba ni yake’’

‘’Baada ya baba kumjibu hivyo,marehemu alikasirika na kuamua kubomoa dirisha la chumba hicho na ndipo baba yake al;ipokwenda kutoa taarifa polisi ambao walifika na kumkamata na waliokuja kumkamata ni mgambo huyo na polisi Simon’’

Hata hivyo alisema,wakati walipokuja kumkamata marehemu hakukubali na walitumia nguvu lakini njia nzima walikwenda wakitukanana kati ya mgambo,polisi na marehemu na ndiyo sababu za kumpiga.

‘’Baada ya kukaidi amri ya askari hao,walimchukua kwa nguvu na njia nzima walikuwa wakitukanana,Kitendo hicho kiliwaudhi askari na mgambo huyo na walivizia mkuu wa kituo hayupo na ndipo walipomtoa sero na kuanza kumshambulia kwa kipigo hadi akazirai huku akivuja damu masikioni na kumrudisha tena sero’’alisema Lukanazya.

Kutokana na kipigo hicho,Mlangila alijeruhiwa vibaya na siku iliyofuata desemba 20 alipelekwa katika zahanati ya Nkome kwa matibabu zaidi na baadaye siku hiyohiyo alihamishiwa katika kituo cha afya cha nzera.

Hata hivyo, baada ya hali ya Mlangila kuonekana kuzidi kuwa mbaya, desemba 24 walilazimika kumhamishia hospitali ya wilaya ya Geita,hadi desemba 31 walipomhamishia katika hospitali ya misheni Sengerema.

Hata hivyo,hali yake ilizidi kuwa mbaya na Januari 4,2015 waliamua kumhamishia katika hospitali ya rufaa ya Bugando ili kupata huduma zaidi kabla ya kukumbwa na mauti hayo Januari 9,mwaka huu.

Hata hivyo katika hali isiyokuwa kawaida,mwili wa marehemu ambao uliwasili jana nyumbani kwao Nkome kwa ajili ya mazishi umechukuliwa leo na kwenda kutelekezwa nje ya kituo kidogo cha polisi cha Nkome baada ya kuwepo kwa tetesi kwamba jeshi la polisi limepanga kuwalinda watuhumiwa hao na kumtoa kafara mzazi wa mtoto huyo ambaye tayari anashikiliwa akihusishwa na mauaji ya kijana huyo.
 
Na VALENCE  ROBERT, GEITA

No comments: