Katika mabadiliko hayo, rais amewapandisha na kuwa mawaziri kamili, mh Jenista Muhagama ambaye amekuwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa bunge, naGeorge Simbachaweni ambaye amekuwa waziri wa nishati na madini.
Harison Mwakyembe amepelekwa wizara ya ushirikiano wa Afrika mashariki, na waziri wa uchukuzi amekuwa Samweli Sitta, huku Wiliam Lukuvi akiwa waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makaazi akichukua nafasi ya profesa Anna Tibaijuka.
Wengine ni Christofa Chiza aliyeteuliwa
kuwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji, Ummy Mwalimu
naibu waziri wa katiba na sheria, Steven Masele amekuwa naibu waziri ofisi ya
makamu wa rais, na Angera Kairuki
ameteuliwa kuwa naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makaazi.
Charles Mwijage ameteuliwa kuwa
naibu waziri wa nishati na madini, huku Bi Anne Kilango Malechela amekuwa naibu
waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi na Merry Nagu ameteuliwa kuwa naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu
wa bunge.
Mabadiliko
hayo ya baraza la mawaziri, yamefanyika baada ya kuondolewa kwa mawaziri wa
wawili wa nishati na madini na ardhi nyumba na makaazi, kutokana na sakata la
fedha za ESCROW.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment