MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 7 January 2015

SERIKALI HAITAKUBALI UZEMBE KATIKA UTEKELEZAJI WA TASAF AWAMU YA TATU WILAYANI MULEBA



Halmashauri ya wilaya ya Muleba mkoani kagera itamekiwa  kuhakikisha inasimamia mpango wa utekelezaji wa TASAF awamu ya tatu wilayani humo ambao umezinduliwa ili kuzinusuru kaya maskini kiuchumi.

Mkurugenzi wa TASAF ngazi ya taifa  Alphonce Kyariga  amesema hayo leo wakati akifafanua malengo ya   mpango huo  wilayani Muleba  ambao utajumuisha halmashauri za wilaya 53 na Muleba ikiwa ni mojawapo  katika  mpango huo.

Kyariga  amesema TASAF awamu ya tatu itatekelezwa kwa  kwa miaka mitatu ijayo wilayani Muleba  na kufikia  kaya 17,000  kwa kuzipatia ruzuku ya fedha wakilengwa watoto chini ya miaka mitano na wanawake wajawazito.

Akizindua mpango huo mkuu wa wilaya ya Muleba Bw  Lambris Kipuyo  amesema viongozi washirikiane kuhakikisha mpango huo unakuwa mkombozi kwa  jamii  bila kuangalia tofauti za kisiasa ama jografia ya vijiji na mitaa.

Kipuyo amesema taratibu za utekelezaji wa mpango ni pamoja na umakini wa wawezeshaji katika kufanya kazi kwa uaminifu na kuzingatia maadili na miiko ya utumishi na familia maskini zihakikiwe na wenyeviti wa vitongoji katika vijiji. 

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Muleba Joseph  Mkude amesema wataalamu  52 wa halmashauri hiyo  wataanza na  kaya  117 katika vijijiji na mitaa  kubaini umaskini katika huduma za Afya elimu na maji na kufanya  tathmini
 

Na Shaban Ndyamkama/ Mwanaharakati.

No comments: