MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 17 February 2015

KAMPUNI INAYOSIMAMIA SOKO LA MKULIMA KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA YASIMAMISHWA NA KESI KUFIKISHWA MAHAKAMANI.

Halmashauri ya Mji wa Kahama Mkoani Shinyanga imekusudia kuifikisha mahakamani, kampuni ya Vumilia Producers Shoping Center inayosimamia soko la wakulima kutokana na kuvunja sheria ya halmashauri  hiyo  baada ya kuanza ujenzi wa soko hilo bila kibali.
Kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mji wa Kahama, Michael Nzingula alisema hatua hiyo wameifikiwa baada ya  kampuni hiyo kukaidi agizo la halmashauri ya...
kuwataka wafanyabiashara  kuondoka katika soko hilo na kuhamia kwenye masoko yanayomilikiwa na halmashauri.
Alisema  kwa sasa wamepeleka zuio la kusitisha  ujenzi wa vibanda katika soko hilo kwani ujenzi unaoendelea katika soko hilo upo kinyume na sheria kutokana na halmashauri hiyo kutangaza kwamba ifikapo Machi mosi mwaka huu wafanyabishara wa soko hilo wawe wameshahamia katika masoko waliyopangiwa.
Nzingula alisema kutokana na  kampuni hiyo kukaidi agizo halali la serikali, hivyo halmashauri kupitia wanasheria wake wanakamilisha taratibu za kuifikisha mahakamani  kampuni hiyo ili taratibu zingine zifuatwe.
Aidha Nzingula aliwataka wafanyabishara  kutoendelea kuwekeza katika soko hilo, na badala yake waende katika masoko waliyoelekezwa na serikali kabla ya  hatua zingine za kuwaondoa hazijatumika.
Hata hivyo uongozi wa Soko hilo, ulikiri kupokea barua ya kusitisha ujenzi huo na kusema kwamba  huo si ujenzi bali ni ukarabati wa mabanda  ambayo yameanza kuchakaa baada ya kudumu kwa muda mrefu.
Mmoja wa Viongozi Aley Shaban alisema, baada ya kupoke abarua hiyo waliamua kusitisha ukarabati huo, huku akisema  soko hilo lipo kisheria kutokana na serikali kulitambua  tangu kuanzishwa kwake.
Mvutano mkubwa bado upo baina ya uongozi wa soko la wakulima, na halmashauri ya mji wa Kahama kuhusiana na kuvunjwa kwa soko hilo kwa madai kwamba haliingizi  mapato katika halmashauri huku uongozi wa soko ukidai kuwa lipo kisheria.
Na Mwanaharakati.

No comments: