WADAU wa sekta ya kilimo cha pamba
wameshauriwa kutoa elimu ya kilimo cha pamba kwa wakulima wa zao hilo ili
kuongeza uzalishaji.
Wito huo umetolewa jana na
mwakilishi wa Mkuu wa.....
wilaya ya Geita Sashisha Masie ambaye pia ni kaimu katibu tawala wa wilaya, katika semina ya mafunzo kwa wadau wa zao hilo ambapo aliwata wadau hao wajikite zaidi katika kutoa elimu kwa wakulima umuhimu wa zao la pamba.
wilaya ya Geita Sashisha Masie ambaye pia ni kaimu katibu tawala wa wilaya, katika semina ya mafunzo kwa wadau wa zao hilo ambapo aliwata wadau hao wajikite zaidi katika kutoa elimu kwa wakulima umuhimu wa zao la pamba.
“Wito wangu kwenu mkitoka hapa
mkawaelimishe wakulima wa zao la pamba umuhimu wa zao hili na jinsi ya
kuzalisha kwasababu tumeshuhudia uzalishaji wa zao hili umeshuka sana
kutokana na wakulima wenyewe kutolisamini zao lenyewe namatumaini kwamba
mafunzo mliopata yatakuwa ni mkombozi kwa wakulima,”alisema Masie.
“Pamba ni zao muhimu sana ni zao la
biashara hivyo wakulima wakielimishwa vya kutosha na kupewa mafunzo ya kilimo
bora ya zao hili naamini wakulima watalipenda na kulithamini kokote duniani
pamba inategemewa kwasababu inamatumizi mengi,”alongeza Masie.
Naye Meneja mafunzo Joseph Tuku
kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali la Tanzania Gatsby Trust (TGT)
linaloendesha semina hiyo, alisema kuwa shirika lao limejikita kutoa semina ya
mafunzo ya pamba katika wilaya za Sengerema, Nyang’hwale na Geita.
Pia Tuku aliitaka serikali iungane
na shirika la TGT katika utoaji wa elimu na ushauri kwa wakulima wa pamba.
Kwa upande wake Monica Jumbe ambaye
ni mdau na mkulima wa zao hilo alisema amenufaika na mafunzo hayo kwani hivi
sasa ameona umuhimu wa zao hilo pia alisema atakuwa wakala mzuri wa kuelimisha
wakulima wengine.
No comments:
Post a Comment