MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 21 May 2015

KUKAMATWA WATOTO WALIOTAKA KUJIANDIKISHA KYERWA,TAARIFA YA SASA UANDIKISHAJI BVR KATIKA MKOA WA KAGERA



Uandikishaji huo umeanza katika manispaa ya Bukoba, ambapo mtandao huu umetembelea vituo vya mtaa wa Pwani na Nyamkazi kata Miembeni, uswahilini kituo na machinjioni kata Bilele, na kujionea uandikishaji ukienda pole pole, jambo ambalo baadhi ya wananchi wamesema kuwa kama wanaandikisha namna hii yawezekana wananchi wengi wakakosa fursa ya kujiandikisha.
Lewis Josiah, ni mmoja kati ya wananchi waliopo kwenye foleni ya uswahilini, na Bwana Mapula katika kituo cha Nyamkazi wameeleza suala la kusuasua kwa uandikishaji.
Mmoja kati ya wakala kupitia chama cha mapinduzi Hud Idd Miiruko, amesema kuwa wao wanaridhika na uandikishaji, ingawaje wanaenda taratibu sana lakini watamaliza bila matatizo, naye mratibu msaidizi wa uandikishaji manispaa ya Bukoba Bw Abdon Kahwa, amefafanua hali hiyo
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeanza uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura kwa kutumia mfumo wa  kielektroniki wa (Biometric  Voters Registration BVR)  mkoani Kagera katika Manispaa ya Bukoba  leo 21/05/2015 kuanzia asubuhi saa mbili, ingawaje baadhi ya vituo kama Machinjioni uandikishaji umeanza saa3 baada ya mashine kuchelewa kufikishwa.
Kulingana na ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uandikishaji wa wananchi katika mkoa wa Kagera utafanyika kwa siku 29 kuanzia hiyo kesho Mei 21, 2015 hadi Juni 18, 2018 ambapo maoteo ya uandikishaji ni wananchi 1,217,388 kwa mkoa wa mzima.
Wananchi wanaotarajiwa katika Halmashauri hizo ni 92,000 Bukoba Manispaa, Bukoba 148,033, Biharamulo 150,000, Karagwe 130,000, Kyerwa 150,000,  Missenyi 144,600, Muleba 198,600 na Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ni 128,000.
Aidha vituo vya uanduikishaji vilivyoainishwa katika mkoa mzima wa Kagera nia 1,676 ambapo Bukoba Manispaa ni vituo 75, Halmashauri ya Bukoa 250, Biharamulo  140, Karagwe 217, Kyerwa 207, Missenyi 174, Muleba 395,  na Halmashauri ya Wilaya ya Ngara 218.
Wananchi wa mkoa wa Kagera wote wanaokidhi vigezo pia wenye umri wa miaka 18 wanahamasishwa kujitokeza katika vituo vitakavyokuwa katika maeneo yao kujiandikisha ili waweze kupata haki ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Oktoba mwaka huu.
Taarifa ambazo mtandao huu bado unafuatilia, watoto kadhaa wamekamatwa huko Karagwe wakiwa kwenye foleni na haijajulikana kama ni raia wa Tanzania.
Na Mwanaharakati.

No comments: