. Ni baada ya viongozi kuuza ardhi ya Cardinal Rugambwa,
.
Wananchi walilia ardhi kurudi kwao, mmoja asimulia mumewe kufia jela,
.
Ofisi ya mkurugenzi yakili kukiuka maamuzi ya serikali kuu.

Viwanja vya shule ya Rugambwa vimemegwa
na kuuzwa huku baadhi ya maeneo ya wananchi waliozunguka pale navyo kuuzwa,
kama wananchi wanvyoeleza.Katika kipindi cha mwaka 2011 hadi sasa,
manispaa ilianza utaratibu kupima viwanja katika mpango wa utekelezaji Ilani CCM,
ili kupanga mji wa Bukoba kama ilivyosikika kwenye kampeini za mwaka 2010, na hii
ilikuwa nikuunga mkono mapendekezo ya wizara ya ardhi na maendeleo ya makaazi
kuhusu upangaji wa miji.
Katika kutekeleza swala hilo
kumejitokeza mapungufu yaliyosababishwa na halmashauri ya manispaa ya Bukoba,
na kuzua mgogoro ambao mpaka umeigawa manispaa kisiasa, na hasa mbunge wa jimbo
hilo alipoanza kukataa utaratibu uliotumiwa na baadhi ya wataalamu wa manispaa
hiyo chini ya aliyekuwa meya wake Anatory Aman.
Kutokana na wananchi kulalamikia
halmashauri hiyo tarehe 12 may 2015, na kumtaka mbunge wa jimbo hilo balozi
Khamis Kagasheki, kushughulikia tatizo hilo kabla ya uchaguzi mkuu 2015, sauti
ya mnyonge imefika kwa mbunge huyo kusikia anavyoshughulika suala hilo.
Manispaa ya Bukoba kwa sasa ina ramani
ya mwaka 1989, ambayo inaonesha eneo la viwanja vya sekondari pamona kile
kinachoonesha jina la EDUCATION CENTER ambacho ndicho walitaka kuligawia jeshi,
katika kilima cha Kashura, manispaa ilipima viwanja 13 mwaka 1996, ambapo kwa maelezo ya afisa
ardhi msaidizi manispaa ya Bukoba Bwana Kakwezi, viwanja hivyo vilipimwa chini
ya uongozi wa mkoa wa Kagera.
Kwamujibu wa taarifa ya ofisi ya
mkurugenzi manispaa ya Bukoba, viwanja hivyo 13 walipewa wananchi mbalimbali
kuviendeleza japo havijaendelezwa, na sautiyamnyonge imebaini maeneo hayo
kuchimbwa kokoto na uwepo wa miti, lakini manispaa inathibitisha kuwa eneo la
shule lililopimwa 1989 halijavamiwa, kitendo ambacho wananchi wanapinga upimaji
wa mara nyingine kwani vilitengwa tangu 1962, kwa kutolewa na wananchi wa
kijiji Kitendaguro wakati huo, iweje leo viuzwe na manispaa?
Afisa ardhi msaidizi katika ofisi ya
mkurugenzi manispaa ya Bukoba, baada ya kutakiwa athibitishe kauli ya wananchi
na mbunge wa jimbo la Bukoba mjini mbele ya mkutano wa wakaazi wa kata
Kitendaguro, amekiri kufanya makosa, kuwa manispaa haijatekeleza masharti ya
serikali kuu.
Mwezi uliopita, sauti yamnyonge imetoa
ripoti maalumu kuhusu migogoro ya ardhi nchini, na kubaini kusababishwa na
kutofuatwa kwa sheria za nchi, na manispaa ya Bukoba ikiwa miongoniwa
halmashauri zinazoongoza kuwa na migogoro ya ardhi nchini.
Hatahivyo
manispaa ya Bukoba suala la ubadhilifu wa ardhi ya wananchi, yameandikwa na
gazeti laJAMHURI chini ya udhamini wa mfuko wa vyombo vya habari TMF, katika
habari ya tarehe 19 November, 2014, ikiwa na kichwa
cha habari;- Mongela karibu Bukoba, tatua migogoro ya ardhi.
TAARIFA YOTE YA UCHUNGUZI NA WANAOHUSIKA WAKO HAPA CHINI
Wiki tatu zilizopita, Rais Jakaya Kikwete alimteua John Mongela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Wiki tatu zilizopita, Rais Jakaya Kikwete alimteua John Mongela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Mongela anachukua nafasi ya Kanali Fabian Massawe ambaye
uteuzi wake ulipotenguliwa taarifa ya Ikulu ilisema atapangiwa kazi nyingine.
Wapo waliofurahi, na wapo walionuna.
Kwa uzoefu wangu usio mkubwa wa walau miaka zaidi ya 20
katika kazi hii, Massawe ndo ‘ngoma’ imefikia mwisho. Nafahamu Massawe
anapigiwa upatu. Nimemfahamu Massawe siku nyingi kidogo, tangu akiwa Mkuu wa
Shule ya Sekondari ya Jeshi ya Jitegemee, Dar es Salaam.
Namfahamu Massawe akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, baadaye
Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, na hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Kagera. Massawe kila
anapopita migogoro inamfuata. Akiwa Kinondoni, mgogoro wa ardhi Luguruni, Dar
es Salaam haukuwa na kipimo.
Akiwa Karagwe tunakumbuka mgogoro uliofukuta pale hadi
watumishi wa halmashauri wakasimamishwa kazi kwa zaidi ya mwaka, huku aliyekuwa
Mwenyekiti wa Halmashauri Lunyogote akitamba. Alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa
Kagera Massawe pale alivunja rekodi, akashiriki mgogoro wa ardhi Bukoba.
Nikiri kuwa “Baniani” anaweza kuwa mbaya, ila kiatu chake
kikawa dawa. Kabla sijazungumza ya ovyo aliyofanya Massawe, nigusie kwanza zuri
moja angalau. Usafi. Hakika Massawe alijitahidi kuhakikisha Mji wa Bukoba
unakuwa safi. Kichungi cha sigara kilitosha kumpiga faini ya Sh 50,000
aliyekitupa. Mongela hili liendeleze.
Mji ukawa safi. Katika hili nampongeza Massawe. Hata hivyo,
alijiingiza katika vitendo visivyokubalika duniani na mbinguni. Alijiingiza
katika ushirikiano usio mtakatifu na manyang’au. Wazaliwa wa Bukoba Mjini
wakapokwa kila chembe ya haki katika ardhi.
Sitanii, mgogoro wa ardhi unaoendelea katika halmashauri ya
Manispaa ya Bukoba hadi leo una sura nyingi. Zipo tuhuma tisa zinazofahamika
karibu kwa kila mtu, ila pia mazungumzo yaliyofanywa na JAMHURI mjini Bukoba
hivi karibuni yamethibitisha uwapo wa wasiwasi mkubwa katika kila kona ya mji.
Julai 7, 2013 madiwani 15 wa Manispaa ya Bukoba waliandika
barua kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba wakitumia Kanuni Na 80 ya Kifungu
(1) na (2) cha Kanuni za Kudumu za Hamashauri pamoja na Tangazo la Serikali Na.
264 la Mwaka 1995 dhidi ya aliyekuwa Meya, Anatory Amani.
Baada ya kuwezeshwa na Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania
(TMF), JAMHURI lilichunguza na kubaini kuwa tuhuma dhidi ya aliyekuwa Meya
zilianza kupigwa danadana na zikawa zinahamishwa kutoka kwa aliyekuwa Meya
kwenda kwa watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba.
Diwani wa Kahororo, Chifu Adronikus Karumuna aliyelijulisha
JAMHURI kuwa anamuunga mkono Amani, aliweka bayana kuwa waliopaswa kukaguliwa
ni watendaji wa halmashauri na si aliyekuwa Meya, kwani aliyekuwa Meya si
mtendaji. CAG alipofanya ukaguzi alibaini maajabu makubwa.
Sitanii, Mongela ni mmoja kati ya vijana wachapakazi wa
kweli katika Tanzania. Nimemfahamu Mongela kitambo, akiwa Umoja wa Vijana wa
Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na baadaye Mkuu wa Wilaya Kigoma, kisha Mkuu wa
Wilaya ya Arusha. Kote alikopelekwa alikutana na migogoro, lakini ameimaliza.
Kwa Mkoa wa Kagera, tuhuma kubwa iliyomgharimu Katibu wa
CCM, Everine Mushi, Amani na sasa Mkuu wa Mkoa Massawe ni kutaka kupora wakazi
wa Manispaa ya Bukoba ardhi.
Aliyekuwa Meya aliamua kuchukua mikopo bila kibali cha
Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupima viwanja na kuuza. Madiwani waliozungumza
na JAMHURI, walikiri kuwa walishirikishwa katika hatua za awali za kuandaa
miradi hiyo, ila utekelezaji uligeuka wa upande moja.
Sheria ya Serikali za Mitaa ya Mwaka 1982 kifungu cha 51 (1)
– (7) inasema kwa kila mkopo lazima halmashauri ipate kibali cha Baraza la
Madiwani, lakini Meya wa zamani Anatory alikopa Sh milioni 500 zaidi ya kiasi
kilichokubaliwa kutoka UTT bila kupata kibali cha Baraza la Madiwani.
Awali alikuwa amekubaliwa kukopa Sh bilioni 2.4, lakini
akakopa Sh bilioni 2.9. Ukiacha hilo, sheria inataka mkopaji awe Mkurugenzi na
si aliyekuwa Meya.
Sitanii, hadi leo katika eneo hili, kuna malalamiko ya
wananchi kupunjwa fidia kwa kulipwa wastani wa Sh 300 kwa mita ya mraba na
kutakiwa kuinunua mita hiyo hiyo kwa Sh 4,000 baada ya kupimwa. Baadhi ya
viwanja vya wananchi vimechuliwa bila kulipwa fidia, kama inavyokiri taarifa ya
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba aliyehamishwa Hamis Kaputa kuwa
wamilikia 280 ardhi yao ilitwaliwa bila kulipwa fidia.
Soko la sasa la Bukoba lilitakiwa kuvunjwa na kujengwa
jipya. Madiwani 15 walimtuhumu aliyekuwa Meya kuwa alikopa Sh milioni 200
kutoka UTT bila kufuata utaratibu wa kupata kibali cha Baraza la Madiwani.
Aliyekuwa Meya anatuhumiwa pia kusitisha malipo na ushuru wa kila aina katika
soko hilo, akitaka livunjwe ifikapo Januari 15, 2013. Hadi leo halijavunjwa.
Mkopo huu aliuchukua kwa riba ya asilimia 24, na wanadai pia
kuwa aliyekuwa Meya alikopa fedha kiasi cha Sh milioni 450 kutoka Benki ya
Posta, ambazo madiwani walielezwa kuwa sehemu ya fedha hizo ingetumika kulipa
mkopo wa UTT. Wafanyabiashara wa sokoni walifungua kesi kupinga kuvunjwa kwa
soko wakidai hawajashirikishwa.
Sitanii, madiwani walimtuhumu aliyekuwa Meya kuwa ametumia
jumla ya Sh milioni 257 kuanzisha mradi wa kuosha magari, na wakasema taratibu
za zabuni hazikufuatwa katika kutoa zabuni hii eneo la Kishenge. JAMHURI
lilizungumza na wakurugenzi wanaosimamia mradi huo, ikathibitika kuwa taratibu
zilivunjwa.
Madiwani walimtuhumu aliyekuwa Meya kuwa aliteua mkandarasi
wasiyemjua kujenga Stendi ya Mabasi Kyakailabwa katika Kata ya Nyanga, na
walielezwa kuwa mkandarasi alilipwa Sh 135,400,000. Hadi leo stendi imeota
nyasi.
Katika eneo la sasa ilipo stendi ilikubaliwa kuwa ujengwe
mradi wa kisasa wa kitege uchumi kwa kujenga jengo lenye urefu wa ghorofa 10 au
zaidi. Madiwani walisema sheria, kanuni na taratibu za kuanzishwa kwa mradi huu
zilikiukwa.
Aliyekuwa Meya alituhumiwa kufanya uamuzi wa kubadili
matumizi yaliyopitishwa na Baraza la Madiwani kupitia kwenye Kamati ya Fedha na
Uongozi. Kamati hizi zilidaiwa kuongozwa na watu waliomuunga mkonoMeya katika
kila jambo alilofanya. Pia kamati hizi zinatuhumiwa kukopa kwa niaba ya
halmashauri kitu ambacho ni kinyume na sheria.
Sitanii, madiwani walisema miradi mingi ilipitishwa kwa
kauli za mdomo bila kuwapo maandishi yenye kuonyesha mchanganuo wa mradi,
kinyume na kanuni Na 42 Kifungu cha 2 (f) cha Kanuniz a Kudumu za Halmashauri.
Si hayo tu, bali zipo taarifa kuwa Shule ya Msingi Kiteyagwa
ilikuwa na uwanja wa mpira wa miguu ambao ulikuwa unatumiwa na watoto, lakini
kwa sasa aliyekuwa Meya Amani ameuchukua uwanja huo na kujenga majengo ya shule
zake za Amani English Medium Primary School na Peace Secondary School. Uwanja
huu ulikuwa unatumiwa na wanafunzi wa shule za Kiteyagwa, Rwemishasha na
Rwamishenye, na hivyo sasa hawana mahala pa kuchezea mpira.
Sitanii, pia upo mradi wa maji uliopaswa kujengwa kwenye
Kata Nyanga kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, mradi huo aliyekuwa Meya Amani
alituhumiwa kuuhamishia Kagondo Karuguru, lakini la ajabu zaidi tenki la maji
limejengwa kilimani na kuelekeza maji zilipo shule zake za msingi na sekondari,
hivyo wengi wanasema mradi huu aliuhamishia Kagondo si kusaidia wananchi bali
kuwezesha shule zake kupata maji. Baada ya makala nilizoandika mradi huu
ulirejeshwa Kata Nyanga.
Madiwani walimtuhumu aliyekuwa Meya kuwa hesabu zinazotolewa
kwenye muhtasari wa halmashauri zinatofautiana kwa kiasi kikubwa na matumizi
halisi. Kwa mfano, Muhtasari Na. 08/99/29/1/2013 unaonyesha kuwa fedha
zilizotumika katika ununuzi ni Sh 485,269,842, wakati matumizi sahihi ni Sh
32,698,533.33. Wanasema fedha iliyopotea ni Sh milioni 452,571,309.33.
Mihtasari mingi ina upungufu wa kutisha katika tofauti kati ya matumizi
yanayotajwa na matumizi halisi.
Sitanii, kilele cha mgogoro kilikuwa Agosti 14, 2013 wakati
Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera ilipowafukuza uanachama madiwani
Deusdedith Mutakyahwa (Nyanga), Dauda Karumuna (Ijuganyondo), Samuel Ntambala
Luhangisa (Kitendaguro), Yusufu Ngaiza (Kashai), na Murungi Kichwabuta (Viti
Maalum).
Hata hivyo, Kamati Kuu ya CCM ilibatilisha uamuzi huo na
kuagiza ufanyike ukaguzi maalum kwenye halmashauri kubainisha tuhuma dhidi ya
aliyekuwa Meya Anatory Amani. Tuhuma nyingi zilithibitishwa, aliyekuwa Meya
akaenguliwa, Katibu wa CCM akahamishwa Mkoa na sasa Mkuu wa Mkoa amehitimisha
orodha kwa kuachwa nje ya orodha.
Sitanii, nimeyasema haya si kwa nia nyingine, maana
niliishayaandika, bali kumpa fursa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mongela awafahamu
vyema watendaji na ajue sura halisi ya mkoa anaofanyia kazi. Zipo tuhuma za rushwa
na kesi kadhaa zinaendelea, ila kinachotakiwa Kagera ni haki na mengine yote
watayapata kwa ziada.
Mongela karibu Bukoba, karibu Kagera. Ukitenda haki,
historia itakukumbuka. Ukiachagua mkondo wa mtangulizi wako wa kupoka wananchi
wa Bukoba ardhi, tangazo litakalofuata utasikia redioni kuwa utapangiwa kazi
nyingine. Mongela ijenge Kagera, maliza migogoro. Mungu ibariki Tanzania.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment