MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 17 May 2015

TANZIA; MAZIKO YA MWANDISHI FREDDY BAKALEMWA WA RADIO FREE NA STAR TV MBEYA, YAFANYIKA BUKOBA VIJIJINI.


. Alikuwa mwandishi wa radio free na Star tv
. Ameacha mjane na watoto 3
Alifikwa na umauti wiki hii nyumbani kwake mkoani Mbeya, baada ya kulazwa jumanne alipochomwa na mwiba katika shughuli zake za kijamii, na mguu kuvimba kwasababu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu, siku moja baadaye alipelekwa hospitali mjini Mbeya na alipochunguzwa na mganga ilibainika ameshachelewa kupata tiba ya mguu huo kwani sumu ilikuwa imeshaeneo mwili mzima.

Amezikwa kitongojini kwao Kaato, kijijini Katangalala, kata Kaagya tarafa Bugabo, akiacha mjane Rehema Mwogofi na watoto watatu, wakike mmoja mkubwa na wakiume wawili wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka kati 4 na 7.

KUTAZAMA PICHA ZAIDI

 Marehemu Freddy Bakalemwa, alizaliwa tarehe 2 may 1964 Bukoba vijijini, alifariki tarehe 13 may 2015 na kuzikwa tarehe 17 may 2015. Roho yake Mungu aiweke mahala anapostaili Amina. 

Na Mwanaharakati.

No comments: