. Utwaliwaji viwanja
vya Rugambwa waibuliwa na askofu,
. Watoto wa marehemu
waomba Kagasheki awaibie siri aliyomweleza mara ya mwisho.
Maziko ya mzee Samuel Ntabala Luangisa, yamefanyika mtaani
kwao Kitendaguro, ambapo alizaliwa 20 jan 1932, na kuzikwa tarehe 3 Jun 2015, ambapo katika maziko hayo,
viongozi wa kisiasa, kidini na wananchi walijitokeza na kufanya maziko ya
kisasa kupitia kampuni ya Uganda burial Service Ltd.
Walikuwapo waandishi wa habari wa redio, tv na blog
mbalimbali, lakini hali ilivyozoeleka ya kupiga picha katika matukio kama hayo,
wapiga picha wa Tanzania walizuiliwa kupiga picha badala yake ile kampuni ya
mazishi ndiyo ilikuwa na ruksa za kupiga picha wakati wa kutoa salamu za mwisho
kwa marehemu.
Itakumbukwa kuwa manispaa ya Bukoba imekuwa na mgogoro wa
ardhi baada ya kupimwa viwanja zaidi ya elfu 4 katika kata za Kahororo,
Nshambya, na Nyanga ambapo wananchi walilalamika baada ya kukiukwa kwa
makubaliano waliyopewa na halmashauri ya manispaa kuwa watafidiwa kwa mujibu wa
sheria na kupewa kiwanja kimoja.
Marehemu Ruangisa miezi michache kabla ya kifo chake,
kwakushirikiana na Askofu msaidizi jimbo katoliki la Bukoba Dr Method Kilaini, alianza kushughulikia viwanja vya shule ya
sekondari Rugambwa, ambavyo hatahivyo halmashauri ya mji wa Bukoba ilimpa
Kadinali Rugambwa 1962, lakini manispaa ya Bukoba imeanza kuvimega na kuuza
jambo ambalo limekumbushwa na askofu Kilaini kwakuonesha kuitaji msaada wa
utatuzi wake
Mtoto wa tisa kati ya watoto 11 wa marehemu Luangisa, Bi
Mulungi Kichwabuta, alipata nafasi ya kuzungumza neno la watoto na kutoa
shukrani, lakini akasema mbunge wa Bukoba mjini balozi Kagasheki
ambaye alikuwa
rafiki wa karibu sana na marehemu, alimtembelea baba yao siku chache kabla ya
kifo chake, ambapo marehemu aliwaambia watoto wampishe aongee na balozi,
sikiliza alichosema hapa chini
Marehemu Luangisa, alijiunga na TANU baada ya kuacha kazi
ya....................
ualimu wilayani Kwimba October 1 1956, badaye alijiunga na CCM 9 Jan 1977 na kupewa kadi namba A 256965, alipata mafunzo ya kisiasa Mzumbe morogoro, China, Corea, Jappan, Uingereza, Uswizi, Ujeruman magharibi na mashariki na alikuwa mjumbe wa halmashauri kuu tangu 1967.
ualimu wilayani Kwimba October 1 1956, badaye alijiunga na CCM 9 Jan 1977 na kupewa kadi namba A 256965, alipata mafunzo ya kisiasa Mzumbe morogoro, China, Corea, Jappan, Uingereza, Uswizi, Ujeruman magharibi na mashariki na alikuwa mjumbe wa halmashauri kuu tangu 1967.
Alikuwa diwani tangu 1975 hadi 2015 mwenyekiti wa
halmashauri ya mji na hatimaye meya wa manispaa ya Bukoba, alikuwa mkuu wa mkoa
wa kwanza wa Ziwa magharibi na mkoa wa Mara, akawa balozi wa Tanzania China,
Corea na Zaire kati ya 1973- 75 na mwaka huo akawa katibu mkuu wa wizara ya
jeshi la kujenga taifa.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment