MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 9 June 2015

MANISPAA YA BUKOBA YAJENGA BARABARA KASHAI WALIOJENGA BAADA WABOMOLEWA

. Inaanzia Kashai sokoni hadi Katatorwanso,
. Wananchi wapongeza unjezi baadhi waomba muda,
. Ni fedha kutoka mfuko wa barabara. 

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami umeanza katika kata Kashai kwa gharama ya mfuko wa Barabara, imetajwa hakuna fidia kwa waliojenga baada ya kutengwa.
Pamoja na ujenzi huo, uongozi wa manispaa umesema hakuna fidia kwa wananchi walioguswa na upanuzi wa barabara, kwani walishakubaliana nao tangu maombi ya ukarabati yalipopelekwa kwenye vikao vya baraza la madiwani na kukubaliwa mwaka 2013.




Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita moja inatokea Kashai sokoni kupitia zahanati, Katatorwanso hadi mwisho wa barabara, huku ikishuka hadi mafumbo shuleni, kama anavyofafanua diwani viti maalumu CCM.
Ujenzi huo umegusa maeneo kadhaa kutokana na upanuzi uliofanyika ingawaje kwingine hawajafikia, lakini jamii imepewa taarifa kuhusu ujenzi huo na iweze kutekeleza ubomoaji mara moja, ingawa mafundi wanadai wameanza kupokea kero mbalimbali


Ukarabati huo unafanywa na kampuni ya DECA ENTERPRISE LTD ya mjini Bukoba, ingawa mhandisi wa manispaa ya Bukoba amekuwa mgumu kutoa ufafanuzi, lakini akatujuza kuhusu muda wa kuanza na kumaliza ujenzi huo.

Badhi ya wananchi wamepongeza ujenzi huo, huku wengine wakiomba muda zaidi ili wabomoe maeneo yao wenyewe.


Mchakato wa ujenzi wa barabara hiyo, ulianza mwaka 2013, baada ya kuombewa fungu katika baraza la madiwani wa manispaa ya Bukoba, ambapo harakati za asubuhi imemtafuta mwenyekiti wa CCM wilaya Yusuph Gelvaz Ngaiza.





Na Mwanaharakati.

No comments: