MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 21 July 2015

MBUNGE NA DIWANI WAVURUGANA UCHAGUZI MWENYEKITI BUKOBA VIJIJINI

. Wananchi watahabika na barabara,
. Akana kupewa hela mbunge,
. Wasema apewe nafasi nyingine.



Ni katika kata ya Nyakibimbili wilayani Bukoba vijijini kaskazini magaharibi mwa mkoa wa Kagera, katika jimbo analogombea Jasson Rweikiza, huku wananchi wakimuuliza ataomba vipi kura zao ilhali alishindwa kukamilisha barabara inayowafanya kukosa huduma muhimu za matibabu na kusafirisha bidhaa zao za kilimo kupata masoko.

Hatahivyo inadaiwa kuwa mbunge huyo amesikika akisema kuwa barabara hiyo imeshindwa kukamilika baada ya diwani wa kata hiyo SYLVAND LUGALAMULA kukataa pesa za ukarabati wake.

Katika mahojiano maalumu na kandayaziwa blog, diwani wa kata hiyo aliyemaliza muda wake Bwana Sylivand Lugalamula amefafanua kuwa anahisi mbunge huyo amechukia baada ya kushiriki kampeini za kumchagua mwenyekiti wa halmashauri.





Sambamba na tatizo la barabara, wakaazi wa vijiji vya Nyakibimbili, Kitahya Bugengere na Bundaza, wanakabiliwa na huduma ya matibabu huku wakijengewa kliniki na shirika la kiraia WORLDVISION, ambayo hatahivyo haina wahudumua.

Kandayaziwa blog, bado inaendelea kumtafuta mbunge wa jimbo anayemaliza muda wake katika jimbo la Bukoba mjini kupata maelezo yake kuhusu hilo.
Na Mwanaharakati.

No comments: