. Damu hatarini kukosekana.
Kutokana na hali hiyo, serikali ya
mkoa inaangalia namna ya kukabiliana na damu kwa matumizi ya wagonjwa katika
hospitali, baada ya RED CROSS ukijitoa.
Akizungumza na
mwandishi wa kituo hiki, mkuu wa mkoa wa Kagera Bwana John Mongela, amesema
kuwa kujiondoa kwao kunatokana na kumalizika kwa mkataba kati ya serikali na shirika
la msalaba mwekundu(RED CROSS), ambayo ameelezea kuwa ni jambo zito na
linahitaji nguvu za pamoja kwasababu ya unyeti wake hivyo inapaswa kufanyiwa
haraka
Amesema kuwa
wamefanya kazi hiyo kwa kipindi kirefu katika program mbalimbali tofauti na
suala la damu salama, hivyo viongozi na wananchi, ni wakati kukaa pamoja katika
kukabiliana na hali hii.
Taarifa ya
shirika la msabalaba mwekundu Tanzania kwa ufadhili wa serikali ya Marekani CDC,
ambao umekuwa ukikusanya damu kutoka wilaya zote na kupelkwa mwanza kwa upimaji
na kuhakikisha inavifikia vituo vyote vya usambazaji, limetoa taarifa kuwa ufadhili wake kwa TRCS umefikia ukomo October
mwaka huu na RED CROSS kusitisha huduma zake mkoani Kagera.
Kuondoka kwa
red cross kunaipa jukumu serikali kujipanga na kuratibu huduma hiyo bila
ufadhili, na inashauriwa kuwatumia watalaamu ambao wamekuwa wakifanya kazi hiyo
kupitia ufadhili ili wasaidie kwa utalamu wao kupitia bajeti ya serikali kila
mwaka.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment