
Mkuu wa mkoa
wa Kagera John Mongela, amesema kuwa taarifa ya utafiti wa UKIMWI na malaria mwaka
2007, inaonesha kuwa kiwango cha maambukizi ya malaria kwa watoto chini ya
miaka mitano kilikuwa asilimia 41, ambapo utafiti 2011 kilishuka hadi asilimia
9 na 2015 utafiti umeonesha maambukizi
yameshuka kutoka 41% hadi 9.5%.
Pamoja na
kuipongeza taasisi ya utafiti wa malaria RTI, mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa mikoa
tafiti zinaonesha kuwa mikoa mingine ambayo haikuwa na utaratibu wa
unyunyiziaji dawa ya mbu majumbani, kiwango cha malaria kimeendelea kuwa juu,
akitolea mfano mkoa wa Lindi 35.7 kwa kupunguza kiwango kidogo hadi asilimia 29
kwa mwaka, huku Kigoma maambukizi yakipanda kutoka asilimia 19.6 mwaka 2007
hadi asilimia 26 mwaka 2011
Mkuu wa
mkakati wa unyunyiziaji dawa majumbani nchini Stephen Magesa, ameiomba
ofisi ya
mganga mkuu kuongeza nguvu katika vijiji vya kando ya ziwa wilayani Muleba kuwa
na kiwango cha juu cha maambukizi ya malaria, ingawa tathmini yake bado
inafanyika.
Mratibu wa RTI uhamasishaji mkoani Kagera Deodart Ngaiza, amesema unyunyiziaji wa
dawa ya kuua mbu majumbani ulianza mwaka 2007 kwa kushirikisha jamii husika ili kuondoa dhana ya imani potofu iliyokuwa imetawala kuwa zinapunguza nguvu za kiume.
Amewashauri
wananchi kuzingatia maelekezo ya wataalamu katika matumizi ya nyumba
zilizopuliziwa kutumika sambamba na vyandarua wanavyopewa
Mkutano wa
wadau wa utekelezaji huduma za afya mkoani Kagera, umefanyika kwa
kuwashirikisha wakurugenzi wa halmashauri za mkoa, watendaji wa huduma za afya
na waratibu
wa mradi wa unyunyiziaji wa dawa ya kuua mbu majumbani mkoa na taifa.
wa mradi wa unyunyiziaji wa dawa ya kuua mbu majumbani mkoa na taifa.

Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment