Serikali imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi
mkuu kutoa wasemaji wa mwenendo wa siasa katika kipindi chote cha uchaguzi.
Mkurugenzi wa idara ya utangazaji Tanzania, amesema hayo
wakati wa kuchambua kanuni za utangazaji katika vyombo vya habari wakati wa
uchaguzi wa vyama vya siasa hapa nchini, kwenye semina ya siku moja
iliyowashirikisha wakurugenzi, wahariri na waandaaji vipindi wa redio na tv
kanda ya ziwa.
Amesema kuwa kutokana na kupitishwa kwa sheria kuhusu vyombo
vya habari na utangazaji, ni lazima hata vyama vifuate utaratibu elekezi, ili
kutoa fursa pande zote kushiriki kikamilifu huku akisisitiza kuwa hakuna chama
cha siasa au chombo cha habari kitakachoonewa kama sheria na taratibu
zilizowekwa zitafuatwa.
Kwaupande wake afisa mkuu wa utangazaji Tanzania Andrew
Kisaka, amesema kuwa hakuna tatizo la mtangazaji au mwandishi kufanya
mawasiliano na chama cha siasa au mwanasiasa kwa lengo la kupata habari,
ingawaje mwandishi atakayeshiriki kugombea atatakiwa aombe likizo au kuacha
kazi kwa muda wote wa uchaguzi
Amesema kuwa wanasiasa watakaotakiwa kuhojiwa na vyombo vya
habari, watatakiwa kukubali ili kusaidia chombo husika kufanya kipindi chenye
uwiano sawa, kwani atakapokataa haitaondoa chama kingine au mwanasiasa mwingine
kuhojiwa ingawa lazima vyama viwili au zaidi vishiriki kipindi hicho.
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, imetoa semina hiyo kwa
vyombo vya habari kanda ya ziwa, kwa dhamira ya kudhibiti mawasiliano,
kusisitiza kufuata sheria itakayoanza kutumika tarehe 1 mwezi wa 9/2015.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment