MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 25 August 2015

MRATIBU UCHAGUZI AELEZA WALIOENGULIWA KUGOMBEA BUKOBA; FUNGUA SAUTI HAPA


Akuzingumza na mtandao huu, mratibu uchaguzi manispaa ya Bukoba amepokea mapingamizi 10 kutoka kata mbalimbali katika ngazi ya udiwani.

Mapingamizi hayo yamewekwa na wagombea udiwani katika vyama mbalimbali vya siasa, ambapo mratibu wa huyo wa uchaguzi Bw Elick Bazombopora, amesema kuwa mgombea wa kata Kahororo Bw Chief Abdronicas Kalumuna amewawekea mapingamizi wagombea  Venant Lugemalila Salapion wa CCM na Bnyenza Saimon wa  ACT, hatahivyo Bw Banyeza amepeleka pingamizi ambalo haliokutaja linampinga nani.

Mratibu huyo amesema kuwa katika kata Miembeni Pingamizi limewekwa na Baganda Gyeshumba Richard wa CHADEMA akimwekea Richard Gasper, ambapo katika kata Kashai,  mgombea wa CCM Bw Samora Agaptus Lyakurwa, amewekea pingamizi ndugu Kabaju Abdukad, ilhali katika kata Kagondo kuna mapingamizi  matano na mapigamizi matatu yakiwekwa na Anatory Aman kwa wagombea watatu.

Amesema kuwa amewawekea Simart Peter Baitan wa CCM, Joram Ifunya wa CHADEMA, na tatu kwa mgombea wa ACT Benson George Bitegeko, ambapo Joram wa CHADEMA amemwekea Baitan wa CCM, ilhali  Benson George Bitegeko akimwekea Anatory Amani.


Katika barua yake yenye kumbukumbu namba BMC/KT/KAG/A.2/49, amabaye ni msimamizi msaidizi wa uchaguzi kata Kagondo, amesema kuwa ametengua uteuzi wa Dr Anatory Amani kugombea udiwani, kutokana na pingamizi la Bw Benson George Bitegeko wa ACT kuhusu kudanganya eneo alilozaliwa, ambapo katika barua yake Amani alionesha kuzaliwa wilayani Karagwe, ilhali taarifa za mamlaka zinaonesha amezaliwa katika eneo la Kanoni Ruanda, kwenye wilaya ya Rakai nchini Uganda, hivyo hakutoa taarifa sahihi za kuzaliwa kwake.

Kupitia baraua yenye kumbukumbu KSH/UCH/VEO.1/05, iliyoandikwa na msimamizi kata Kashai, imetengua uteuzi wa ndugu Kabaju Nuruhuda Abdukadir kugombea udiwani kwenye kata hiyo kwasababu ya pingamizi alilowekewwa na mgombea wa CCM ndugu Samora Agapmtus Lyakurwa.
 
Na Mwanaharakati.

No comments: