MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday 26 August 2015

TASAF KUTOHUSIKA KUWATAMBUA MASKINI, SOMA NA SIKILIZA HAPA



Katika awamu ya tatu ya mfuko wa kaya maskini nchini, mkoani Kagera wameendelea na utaratibu wa ugawaji fedha katika kaya husika, ambapo jumla ya mil 319,060,000/= zinazotolewa kwa   walengwa 8753 Bukoba vijijini, na kiwango cha chini ni sh 20,000/= ilhali cha juu kikiwa ni sh 86,000/= kulingana na ukubwa wa familia.

Mtandao huu umeshuudia mchakato wa utoaji fedha kwa baadhi ya kaya kwenye kata za Bujugo na Karabaige, kando na hiyo kumekuwa na malalamiko juu ya mfuko huo, ikitajwa kuwa wanaopewa siyo wahusika yaani ni wale wanaojiweza na wasio jiweza kuwekwa kando.
Ismail Hamidu ambaye ni afisamratibu wa TASAF halmashauri ya Bukoba vijijini Bw Ismail, amesema kuwa wao hawahusiki  kufanya mchakato wa utambuzi kuhusu maskini, badala yake ni viongozi wa vitongoji na mitaa ambao wanaishi karibu na wahusika, ambapo taarifa zao ndizo zinawezesha kuwapa mgawo sawa kulingana na ukubwa wa kaya. 
Amesisitiza kuwa TASAF haihusiki kutambua kaya maskini bali ni kazi ya wanavijiji au mitaa husika na wao hupewa taarifa baada ya kukidhi vigezo vinavyotolewa na TASAF, hivyo malalamiko yanayojitokeza siyo ya msingi.

Amesema kuwa awali kulikuwa na wakati mgumu kuwapata wahusika, kwasababu kulikuwa na uvumi kuwa fedha hizo ni za FREEMASON lakini baada ya kugundua siyo kweli, wamejikuta wakitaka kuingizwa kwenye mchakato ilhali hawakuudhuria mikutano ya utambuzi, ndiyo maana kuna baadhi ya malalamiko kuwa wamebaguliwa.


Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Bukoba Bi Jenista Lugakingira, amesema kuwa serikali inaendelea kutekeleza mipango yake kwa wananchi, kwani inatambua umuhimu na mahitaji katika kusukuma mbele maisha yao, huku akiwasihi kujitokeza kupiga kura kumchagua kiongozi wanayemtaka, ifikapo oktoba 25 mwaka huu.

Na Mwanaharakati.

No comments: