MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 8 September 2015

MAKUBWA KATIKA MIKUTANO YA CCM NA UKAWA MANISPAA YA BUKOBA.


. Mkapa asisitiza mabadiliko yaliyofanywa na ccm,

. Kagasheki siwezi kupoteza muda kujadili matusi,
. Rwakatare asema naye alete mke wake,
. Wapambe wa Lowasa wamkana.
Mikutano miwili imefanyika katika manispaa ya Bukoba ikihusisha CCM na UKAWA, ambapo katika uwanja wa mashujaa Mayunga, rais mstaafu Benjamin Mkapa, ameongoza wanaccm kuzindua kampeini za chama hicho mkoani Kagera.
Kwa niaba ya wagombea ubunge ccm katika mkoa wa Kagera, Bw Mwijage ambaye anagombea jimboni Muleba, amesema kuwa waliokuwa wanachafua ccm wameondoka baada ya kunyimwa nafasi na wengine wamefukuzwa, hivyo wameamua kuleta mabadiliko ya kweli kwasababu waliokuwa wakikwamisha ndiyo walioondolewa.

Balozi Kagasheki, amesema kuwa baada ya uzinduzi uliofanyika, atafanya kampeini kwa kuzungumzia matatizo yanayowakabili wananchi, kwani waliokuwa wanaleta shida wameondoka na hayuko tayari kujibizana nao kwasababu majibizano na matusi, siyo utatuzi wa matatizo ya wanyonge.
Kwa upande wao UKAWA kupitia mgombea ubunge Wilfred Muganyizi Rwakatare, amesema kuwa wapewe nafasi nyingine kwani aliwahi kuwa mbunge wa jimbo hilo, ila akipata nafasi anaweza kufanya vizuri kwasababu ameshajifunza.
Wapambe wa mgombea huyo kupitia UKAWA, wamesema kuwa wanapanda jukwaa kumshughulikia Kagasheki pekee kwa kutaja mambo mbalimbali binafsi yanayomuhusu mgombea huyo kupitia CCM.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: