MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 3 September 2015

MVUA ZA SABABISHA MAHAFA KARAGWE- UNDANI UKO HAPA.



Taarifa kutoka Karagwe mkoani Kagera, zinasema kuwa mvua  zilizonyesha  Agosti  30  na  31 mwaka  huu  katika  kata  ya  Bugene  zimesababisha  maafa  katika  kijiji   cha  Kishao  baada  ya  migomba  kuangushwa  na  upepo  mkali  na  kuna  baadhi  ya  nyumba  nazo  zimebomolewa  na  mvua  hizo.
Afisa  Mtendaji  wa Kata  Bugene  Bw. Deus  Ntinchwa  amesema  kuwa  maafa  yaliyosababishwa  na  mvua hizo, zilizoanza kunyesha  majira ya saa kumi na moja jioni, na kusema kuwa jumla migomba iliyoanguka ni 58,365,nyumba zilizoezuliwa paa ni 15,na zilizoharibika sehemu ndogondogo ni 9,na mihogo iliyoharibika ni1661.

Kutokana na mahafa hayo,  wananchi  wametakiwa  kupanda  mazao  kwa  wakati  na  kutakiwa  kuchukua  tahadhari  juu  ya  watoto  wao  kipindi  hiki  cha  mvua  za  vuli  zilizoanza  kwa kasi kubwa.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: