MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 2 September 2015

SILAHA ZA KIVITA ZATELEKEZWA KAGERA-MSAKO POLISI WAENDELEA



. Mmoja ashikiliwa kwa mauaji.

Taarifa ya polisi mkoani Kagera juu ya tukio hilo na la mauaji, inasema kuwa wanaendelea kuwatafuta watu watatu kwa tuhuma za kutelekeza begi lililokuwa  na silaha za kivita.
Kamanda wa polisi mkoa humo Agustino Olomi , mesema kuwa tukio hilo limetokea tarehe 1 mwezi Septemba mwaka huu karibu na  kituo kidogo cha polisi Kalenge wilayani Biharamlo, baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema  waliokuwa wakisafiri kutoka Kibondo Kwenda Kahama kuwa kwenye gari lao kuna watu watatu wanawatilia mashaka.

Amebainisha kuwa,watu hao baada ya kutelekeza begi hilo wametokomea polini na jeshi la polisi linaendelea kuwasaka ili kuwabaini.

Hatahivyo  polisi mkoani Kagera inamshikilia mwendesha pikipiki mmoja baada ya kumgonga mtembea kwa miguu na kufariki dunia.
Mtuhumiwa huyo ametajwa na polisi kuwa ni Siliakus Almachius mwenye umri wa miaka 22 na aliyefariki ni Anacreti Anastazi mwenye umri wa miaka 40 mzaliwa wa Karagwe.

Kamanada Olomi amesema kuwa,baada ya ajali hiyo kutokea,mwendesha pikipiki huyo alitoroka lakini baadae  polisi  walimpata, na kuwa  mtuhumiwa huyo muda wowote atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: