MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 1 September 2015

SOMA UNDANI; KAGASHEKI ALIVYONUNUA KIWANJA CHA SHULE BUKOBA

. Pia aliweka miundombinu kadhaa,
. Uzio wahitajika kudhibiti wanafunzi,
. Wanafunzi watumika kuvua samaki.

Ni miaka mitano sasa tangu shule ya sekondari Lutunga kuanzishwa, ambapo ufaulu wa kwanza wa kidato cha nne mwaka jana 2014 wanafunzi wanne walichaguliwa kujiunga kidato cha tano, kati ya wahitimu 48.

Mwandishi wa mtandao huu ametembelea shule hiyo na kutajiwa changamoto, ya
ukosefu wa uzio, upungufu wa nyumba za walimu, uhaba wa huduma ya maji, na mahitaji ya huduma ya umeme, kama alivyofafanua Madam Hawa….



Kwa mujibu wa uongozi ndani ya kata Kahororo manispaa ya Bukoba, shule hiyo ilanzishwa baada ya mbunge anayemaliza muda wake Balozi Khamis Kagasheki, kununua kiwanja ili wajenge shule hiyo, kwa wakaazi baada ya kupendekezwa kwa eneo husika, na kuchangia ujenzi wa shule hiyo, ambayo hadi sasa ina madarasa 4 ikiwa bado na uhitaji wa madarsa 4 ili kukamilisha mikondo miwili inayotakiwa kuwa katika shule hiyo na kukidhi mahitaji ya wanafunzi zaidi 160 waliopo shuleni hapo.

Na Mwanaharakati.

No comments: