MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 27 September 2015

TAARIFA MPYA KAMILI UCHOMAJI MAKANISA SASA NI BUKOBA VIJIJINI

Ni makanisa mengine matatu ya Rc, na KKKT mawili ambapo taarifa inasema kuwa kanisa la Romani katoliki kigango cha Kiijongo kata Katoro, na makanisa ya kata Kaibanja na la kitongoji cha Musila kata Katoro Bukoba vijijini.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Augustine Ollomi amesema kuwa watu wasiofahamika wamevamia makanisa hayo na kukusanya vifaa kama biblia, bahasha za sadaka, majoho na ngoma na kuvichoma moto.

Amewasihi waamini, viongozi wa dini na wananchi, kutoa ushirikiano kwa mamlaka, ili wafanikishe kukamata wahusika.

September 22 mwaka huu, makanisa matatu ya kipentekoste katika manispaa ya Bukoba, yalichomwa moto na kusababisha hasara ya shilingi milioni 12.9.

Na Mwanaharakati.

No comments: