Ni baada ya kukamilisha na kuzindua shule
ya Sekondari JK Nyerere pamoja na nyumba za walimu, kwa gharama ya shilingi
bilioni 1.7 wilayani Tarime.
Ujenzi wa shule hiyo iliyopo kijiji
cha Nyamwaga kinachopakana na mgodi huo umeenda sambamba na ununuzi wa
samani za ofisi za walimu, madarasa na maabara.
Meneja wa Mgodi huo unaomilikiwa na
kampuni ya ACACIA, Jimmy Ijumba amesema shule hiyo imejengwa kwa
awamu ambapo kwasasa zimekamilika awamu mbili ambazo wigo wake ni madarasa
nane, nyumba za walimu sita zenye vyumba vya kulala vitatu, stoo, jiko, bafu,
tanki la maji pamoja na uzio, jengo la utawala, maktaba, maabara mbili, vyoo
vya walimu na wanafunzi vyenye matundu 33.
Aidha Mgodi huo umenunua kompyuta za
wanafunzi na walimu, photocopier machine, printer, projector na scanner kwa
ajili ya shule hiyo.
Alifafanua kwamba ujenzi wa shule
hiyo umekuwa ukitekelezwa kwa awamu kutokana na shule kuwa mpya kwani ina
kidato cha kwanza na cha pili na kama majengo yote yangejengwa kwa wakati mmoja
yangekosa matumizi.
“Awamu ya tatu ya ujenzi wa shule
hii utatekelezwa mwakani kwa kuhusisha madarasa manne, bwalo la chakula na
chumba cha kupumzikia wagonjwa”, alisema Ijumba.
Kwa upande wake Mama Kikwete
aliipongeza kampuni ya ACACIA kwa kuchangia jitihada za Serikali za
kuboresha elimu kwa watoto na kusema kuwa mfano huo unapaswa kuigwa na
makampuni mengine hapa nchini.
Alisema njia pekee ya kupambana na
ujinga, maradhi na umasikini ni kuwapeleka watoto shule kwani wao ndiyo tegemeo
la wazazi, nguvu kazi na rasilimali ya taifa.
Wakielimishwa watakuwa
wanawatengenezea njia ya kujikomboa katika Nyanja za kijamii na kiuchumi na
watakuwa msaada mkubwa kwa wazazi wao pindi watakapokuwa wazee.
Mradi wa ujenzi wa shule ya JK
Nyerere ni moja kati ya miradi ya kijamii katika kijiji cha Nyamwaga
inayotekelezwa kwa ufadhili wa mgodi kama ilivyoainishwa kwenye mkataba
wa manufaa ya vijiji (VBIA) uliosainiwa kati ya mgodi na kijiji mwezi Februari
2012.
Miradi mingine ni ya sekta ya maji,
afya, elimu, barabara za jamii, umeme na uchumi.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment