MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 9 November 2015

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA RAMANI YA ZAMANI


.Haioneshi marekebisho ya mikoa mipya,
.Wachapishaji wauzaji kukamatwa,
.Yasema hakuna mgogoro na Malawi.


katika baadhi ya maeneo.
Mkurugenzi wa habari maelezo ambaye ni msemaji wa serikali ASSAH MWAMBENE, amesema kuwa serikali ilizindua ramani mpya na sahihi, ambayo inaonesha uwepo wa mikoa mipya ya SIMIYU, GEITA na MANYARA, pamoja na kuonesha mipaka ya eneo la ziwa Nyasa na Tanganyika.
Amesema kuwa siku za karibuni baadhi ya vyombo vya habari yakiwamo magazeti ya Mzalendo, Citizen, Mwananchi na Wajibika yalitumia ramani isiyosahihi katika taarifa zake, na serikali inaweza kuvichukulia hatua kwa mujibu wa sheria wakati wowote.
Wakati huo huo, amezungumzia mgogoro wa ziwa Nyasa  kati ya Tanzania na Malawi, kuwa ukubwa wa Tanzania ni pamoja na eneo la ziwa Nyasa, kwani  Malawi ina eneo lake katika ziwa hilo na hakuna mkanganyiko tena kwani Tanzania inahudumia eneo lake na Malawi la kwake kwasababu nchi zilikwisha kaa pamoja na kutoa maelezo na shughuli zinaendelea kawaida.
Itakumbukwa kuwa ramani ya Tanzania, afrika na dunia imekuwa ikiuzwa kiholela na wafanyabaisha mbalimbali nchini, jambo ambalo serikali imewataka kufuata taratibu za upatikanaji wa ramani iliyo sahihi kwenye mamlaka husika, kama wanataka kuendelea na biashara hiyo.

Na Mwanaharakati.

No comments: