MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 29 May 2017

HII NDIYO TAARIFA YA WATATU KUZAMA KWENYE SHIMO LA MAJI BUKOBA

Ni tukio la kusikitisha lililotokea jana baada ya watoto wawili kudumbukia kwenye shimo ambalo lilitumika kutoa changarawe katika mtaa wa Bugambakamoi kata Kitendaguro manispaa ya Bukoba.

Watoto hao ni wanafunzi wa shule ya msingi Kitendaguro na mwili wa mtoto mmoja umeshaopolewa huku kijana mwingine mtu mzima na mtoto wa pili haijaopolewa ilhali polisi, zimamoto na wananchi wanaendelea kutafuta miili hiyo au kuwapata wakiwa salama.

Baada ya harakati za baadhi ya wananchi kuwaopoa hapo jana mapema kugonga mwamba, kijana ambaye hajaonekana alilazimika kuzama kuwatafuta huku wenzake wakimzuia kuingia kwy shimo hilo, anasadikiwa kuwa na umri wa miaka 32 na watoto mmoja ana miaka 14 na wa pili miaka 12, picha za tukio hilo na undani zaidi unaletwa kwenu punde....

Na Mwanaharakati.

No comments: