MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 22 May 2017

MAHOJIANO JUU YA MAUAJI KAGERA HAYA HAPA



Mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Kizilamuyaga kata  Kimwani wilayani Muleba, ameuawa kwa kushambuliwa na kitu chenye ncha kali.

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu kwa njia ya simu, mwenyekiti wa kijiji cha Kizilanuyaga Bw. Adrian Philipo,  amemtaja mwanamke huyo kuwa ni Ester Anaseti mwenye umri wa miaka 30, ambaye anasadikiwa kuuawa na mtu anayesadikiwa kuwa shemeji yake ambaye jina lake limehifadhiwa, usiku wa kuamkia jana jumapili.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Agustine Olomi, amesema hajapokea taarifa za mauaji hayo  na  ameahidi kutoa taarifa kamili baada ya kupokea  undani wa tukio hilo, kutoka kwa mkuu wa polisi wa wilaya ya  Muleba.


Na Mwanaharakati.

No comments: