MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 29 May 2017

MPANGO WA SERIKALI JUU WANAOINGIZA MIFUGO KWENYE HIFADHI ZA MISTU




Waziri wa maliasili na utalii Prof.Jumanne Magembe leo amefanya ziara yake ya siku moja mkoani Kagera kwa lengo la kueleza msimamo wa serikali juu ya wanaoingiza mifugo katika hifadhi za mistu na mapori ya akiba.

Akiwa wilayani Biharamulo Prof.Magembe amesema kuwa hawataruhusu tena mifugo kurudi ndani ya hifadhi,na watahakikisha ndani ya wiki mbili au tatu wanapitisha ndege zenye rubani na ambazo hazina rubani ili kuhakikisha hakuna mtu anayeingiza mifugo ndani ya hifadhi hizo.

Aidha amesema kuwa wakikuta mtu ameingia kwenye hifadhi,watamuondoa pamoja na msimamizi wa eneo hilo na familia yake yote  ili mbegu mbaya isibaki katika kuhifadhi wanyamapori.
 


Na Mwanaharakati.

No comments: