MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 18 May 2017

KAULI NZITO ZA MADEREVA BUKOBA BAADA YA BARABARA ILIYOKUWA IMEKATIKA KUANZA KUTUMIKA.


Mnamo may 12 mwaka huu barabara ya kemondo iliyopo halmashauli ya wilaya Bukoba ilikatika kutokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo na kukatisha mawasiliano kwa wanaotegemea barabara hiyo hususani magari ya kutoka Bukoba mjini kuelekea mikoani na wilaya jirani kama Muleba ambao walilazimika kupitia barabara ya Katerero,Kyetema na Kanyinya.



Barabara hiyo iliyokuwa ikiendelea na ukarabati leo imeanza kutumika kwa magari yote,ambapo baadhi ya madereva wameipongeza serikali kwa jitihada ilizozionyesha kwan awali walikuwa wanapata changamoto kubwa kutokana na msongamano wa magari katika barabara waliyokuwa wakitumia huku wakisubili ukarabati ukamilike.

Aidha wameishauri serikali kukarabati barabara ya Katerero-Kyetema-Kanyinya maana imeharibika sana kwa kipindi ilichotumika na inaweza kusababisha changamoto nyingine kwa wakazi wanaoendelea kutumia barabara hiyo.

Kwa upande wake meneja wa TANROAD mkoa wa Kagera mhandisi Andrew Kasamwa amesema kuwa barabara hiyo ya Kyetema-Kanyinya imekuwa ikiendelea kutumika katika kipindi hiki cha mpito, ingawa, tayari wameshaanza ukarabati wa maeneo yaliyoharibika.

VIDEO YA BAADHI YA MADEREVA  …………………......


Na Mwanaharakati.

No comments: