Mnamo may 12 mwaka huu barabara ya kemondo iliyopo halmashauli ya wilaya Bukoba ilikatika kutokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo na kukatisha mawasiliano kwa wanaotegemea barabara hiyo hususani magari ya kutoka Bukoba mjini kuelekea mikoani na wilaya jirani kama Muleba ambao walilazimika kupitia barabara ya Katerero,Kyetema na Kanyinya.

Barabara hiyo iliyokuwa ikiendelea na ukarabati leo imeanza
kutumika kwa magari yote,ambapo baadhi ya madereva wameipongeza serikali kwa
jitihada ilizozionyesha kwan awali walikuwa wanapata changamoto kubwa kutokana
na msongamano wa magari katika barabara waliyokuwa wakitumia huku wakisubili
ukarabati ukamilike.
Aidha wameishauri serikali kukarabati barabara ya
Katerero-Kyetema-Kanyinya maana imeharibika sana kwa kipindi ilichotumika na
inaweza kusababisha changamoto nyingine kwa wakazi wanaoendelea kutumia
barabara hiyo.
Kwa upande wake meneja wa TANROAD mkoa wa Kagera mhandisi
Andrew Kasamwa amesema kuwa barabara hiyo ya Kyetema-Kanyinya imekuwa ikiendelea kutumika katika kipindi hiki cha mpito, ingawa, tayari wameshaanza ukarabati wa maeneo
yaliyoharibika.
VIDEO YA
BAADHI YA MADEREVA …………………......
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment