MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 12 June 2017

ILIVYOZINDULIWA KWAYA YA TUMAINI JIPYA KASHURA



BUKOBA                                                                                                                            

Kwaya ya Tumain Jipya ya kanisa la Lutheran Kashura lililopo ndani ya manispaa ya Bukoba imeezindua album yake jana  kwa mara  ya kwanza tangu ilipoanzishwa mwaka 2012 ikiwa na wanakwaya kumi na wanne.
Kufikia jana kyaya hiyo ilikuwa tayari na wanakwaya 29,na wamefanikiwa kurecord album yao kwa gharama ya Tsh millioni 6,ambapo katika uzinduzi huo wamebainisha changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni uhaba wa fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya kuendeleza kwaya yao ambayo ni kiasi cha shilingi milioni nane laki moja na elfu hamsini.

Akizindua Album hiyo meya wa manispaa ya Bukoba Chief Kalumna,amewapongeza kwa kujitoa kuubili injili kupitia nyimbo ikiwa ni sambamba na kuwawezesha zaidi ya laki nne huku akiongoza alambee kwa wadau na washirika katika kuwezesha kwaya hiyo.

Kupitia alambee hiyo wamefanikiwa kupata fedha taslimu Tsh.milioni mbili laki mbili na elfu tatu na ahadi ya shilingi millioni mbili na elfu ishirini na tisa.       


Picha za matukio mbalimbali katika uzinduzi huo…………………………………………………………………………..



Na Mwanaharakati.

No comments: