Waziri wa fedha na Mipango Philp Mpango, amemweleza rais Magufuli kuwa
amechoshwa na serikali kuwa ombaomba.
Dr. Mpango amesema hayo wakati
wa uzinduzi wa mfumo wa ukusanyaji kodi kwa njia ya kielektroniki jijini Dar es salaam, ambapo rais Magufuli alikuwa mgeni rasmi, kuwa haiwezekani serikali ikaendelea kuomba mikopo ya kutekeleza mambo
yake ambayo hatahivyo, yangeweza kutekelezwa kupitia fedha zake za ndani.
Amesema kuwa ili kuhakikisha hilo, kama waziri atahakikisha anasimamia
mfumo huo unaozinduliwa leo ili uweze kuongeza ukusanyaji wa mapato nchini.
Mfumo huo ulianzishwa mwaka 2015 kwa kumwezesha mlipa kodi kulipa
katika benki mbalimbali kupitia simu ya kiganjani, pamoja na wa forodha
unaowezesha kulipia mizigo maeneo ya forodha kwa lengo la kurahisisha ulipaji
wa kodi ya mizigo kwenye ofisi ya forodha, ili kuondoa ukwepaji wa kodi na kuisbabaishia
serikaili hasara, kwani inategemea mawasilisho ya makadirio kutoka kampuni
husika, ili kutoipunja serikali au kuwapunja walipa kodi.
Akitoa taarifa ya mfumo huo, kamshina mkuu wa mamlaka ya mapato nchini
TRA Charles Kicheere, amesema kuwa utakuwa
unakusanya ongezeko la thamani, kutoka kwenye mialama mbalimbali, kuahikikisha
kodi inakaridiwa na kufikishwa kwenye mamlaka husika.
Hotuba ya rais wa jamhuri ya Muungano inaendelea katika uzinduzi huo
kwenye ofisi kuu ya mfumo wa ukusanyaji kodi ya TRA Kijitonyama jijini dare s
salaa, ambao umeudhuriwa na rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la
mapinduzi, makamu wa rais Samiah Suluhu Hassan, waziri wa fedha na viongozi
mbalimbali wa kisiasa na dini.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment