MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 1 June 2017

UPDATES; WAZIRI KUFUNGA WIKI YA MAZIWA

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Tayari amewasili Mkoani Kagera katika Kilele cha Wiki ya Maziwa, Maadhimisho ambayo yamekuwa yakiendelea Takribani wiki nzima sasa, katika Manispaa ya Bukoba katika viwanja vya Kyakairabwa.

Maadhimisho haya yanayofanyika Kitaifa Mkoani Kagera, ni  kwa mara ya 20 sasa ikiwa ni mfulululizo tangu kuanzishwa kwake Kitaifa nchini, chini ya Usimamizi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB), ambao ndio waandaaji.
Baada ya kuwasili uwanja ndege na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh, Deodatus Kinawiro, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, msafara umeelekea Viwanjani Kyakairabwa ambapo huko ndipo shughuli inapofanyika.
Waziri Tizeba, mara baada ya kuwasili viwanjani hapo, amepokea maandamano ya wadau wa maziwa wakiongozwa na wanafunzi pamoja na walimu wao kutoka shule mbalimbali za manispaa ya Bukoba, kisha kuanza kukagua na kutembelea mabanda mbalimbali.

Na Mwanaharakati.

No comments: