MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 1 June 2017

VIFO 130 HUTOKEA TANZANIA KWA WATOTO CHINI YA MIAKA 5;Waziri Tizeba



BUKOBA                                                                                                       

Ikiwa leo ni kilele cha wiki ya maziwa kitaifa ambapo imefanyika mkoani Kagera katika viwanja vya Kyakairabwa manispaa ya Bukoba,huku waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi Dr.Charles Tizeba akihitimisha maadhimisho hayo kwa niaba ya makam wa Rais Samia Suluhu.

Akisoma hotuba kwa niaba ya makamu wa Rais,Dr.Tizeba amesema kuwa pamoja na Tanzania kuwa na idadi kubwa ya uzalishaji maziwa bado unywaji wa maziwa umeendelea kuwa mdogo ambapo mtanzania mmoja unywa lita 47 kwa mwaka badala ya lita 200,jambo ambalo linapelekea kuwepo ongezeko kubwa la magonjwa ikiwa ni pamoja na lishe duni.

Dr.Tizeba amesema  kuwa nchini Tanzania imedhihirika kuwa vifo 130 kwa watoto wa chini ya miaka mitano hutokea kila siku kutokana na lishe duni,hii ni kwa mujibu wa taarifa ya UNICEF kwa mwaka 2013.

Mbali na kuhitimisha maadhimisho hayo amezindua operation inayoitwa jenga jahazi,jenga afya,jenga uchumi kupitia maziwa ambayo ina lengo la kuendelea kuhamasisha watanzania kunywa maziwa ili kupunguza tatizo la udumavu wa mwili na akili hususan kwa watoto wetu.

Sanjali  na hayo amekabidhi vyeti,medali na vikombe kwa waliofanya vizuri katika maadhimisho ya awamu hii na mshindi wa jumla ni Kampuni ya ASAS DAIRIES LTD kutoka Iringa ambao mpaka sasa wamekuwa washindi mara tano mfululizo katika maadhimisho ya wiki ya maziwa.

 
Baada ya kuibuka mshindi wa jumla,mkuu wa Kampuni hiyo ya ASAS DAIRIES Lipita Memila amesema kuwa pamoja na kuendelea kufanya vizuri katika bidhaa zao,bado wanasaidia jamii kupitia kile wanachokipata ikiwa ni pamoja na ujenzi wa wodi katika hospitali mbalimbali na huduma nyingine za kijamii.





 BAADHI YA PICHA NDANI YA KILELE CHA WIKI YA MAZIWA KITAIFA
Maandamano ya wanafunzi na wadau mbalimbali  katika kilele cha wiki ya maziwa 2017

Add caption
Waziri akikagau baadhi ya kazi za washiriki



 Waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi akinywa maziwa

Na Mwanaharakati.

No comments: