MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 3 June 2017

SABABU ZA VIONGOZI WATATU WA CHADEMA KUHAMIA CCM MULEBA.



MULEBA  
 By Lameck Richard


Kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika kata ya Kalambi jimbo la Muleba kusini chini ya Diwani wa kata hiyo,Felix Bwahama umekuwa na matukio mbalimbali likiwemo la  viongozi wa vijiji na kitongoji  kutoka Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kuhamia chama cha mapinduzi  CCM.

Viongozi waliohama ni pamoja na mwenyekiti kijiji kalambi Anton Bajuza,mwenyekiti kijiji Kanyamita Mseveni Kazinja na mwenyekiti wa kitongoji Bushabo Sebastian Rutakakwa,ambapo wamesema kuwa sababu kubwa za kuhamia CCM ni kutokana na uongozi mzuri walionao wa diwani wao pamoja na ushirikiano mkubwa wa maendeleo wanaoupata kutoka kwa diwani,mbunge pamoja na Rais.

Kufuatia kitendo hicho Katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Muleba Anatory Nshange amewapongeza kwa hatua hiyo ya kuamua kuungana na chama tawala katika kuwaletea wananchi maendeleo huku akimuagiza katibu wa ccm kata Kalambi kujadili haraka  majina ya watu hao ili waweze kupatiwa kadi za chama rasmi.

Sanjali na hayo Diwani wa kata hiyo Felix Bwahama,amezitaja shughuli za maendeleo ambazo wamefanikiwa kutekeleza ndani ya kata yake kwa kushirikiana na wananchi pamoja na wafadhiri mbalimbali kuwa ni pamoja na kukarabati miundombinu katika shule za kata hiyo,zahanati,umeme vijijini na kufanikiwa kupata barabara ya rami km 10 kutoka Kimea-Nyamilanda.

Kwa upande wa wananchi wamebainisha changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na ukosefu wa maji katika kata yao hali inyopelekea kufuata maji kwa umbali mrefu na kusababisha shughuli nyingine za maendeleo kukwama.

Aidha wameongeza kuwa wanaiomba serikali iwape idadi ya mifugo wanayotakiwa kuwa nayo kama wafugaji na kutengewa maeneo ya kuchungia ili kuepukana na adha ya kuvutana na serikali  kila wakati.
Bw.Bwahama amesema kuwa watendaji wa kata na vijiji wahakikishe wanasimamia vyanzo vya maji kwa ukaribu na wasiruhusu mtu mmoja kuharibu vyanzo hivyo kwa sababu maji ni changamoto kubwa na yanategemewa na watu wengi,huku akisema kuwa bado anaendelea kupambana katika halmashauri ili wajengewe visima vya chini na tayari kuna kijiji kimeshawekwa kwenye mradi.

Pia amewasihi viongozi na watendji wa kata hiyo kutojihusisha na vitendo vya rushwa katika kutekeleza wajibu wao na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano pindi wanapokumbana na changamoto hiyo ili hatua ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

TAZAMA HAPA KWENYE VIDEO ALICHOKISEMA DIWANI WA KATA KALAMBI


Na Mwanaharakati.

No comments: