Rais wa jamhuri ya muunganio wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli, amesema kuwa haiwezekani watu wa halmashauri ya Biharamulo wakaendelea kutekeseka wakati serikali imeshawawekea mazingira bora ya miundombinu, hivyo viongozi wachache wanatakiwa kuwajibika na wakishindwa ni bora wakajiondoa wenyewe.
Akihutubia mkutano wake katika ziara ya kikazi wilayani Biharamulo, rais Magufuli amemtaka mkurugenzi wa maji safi na usafi wa mazingiria Bukoba BUWASA, ambaye ndiye mkurugenzi anayesimamai upatikanaji wa maji katika halmashauri zinazosimamiwa na serikali katika miundombinu hiyo, kufikia julai 30 mwaka huu awe amefanikisha upatikanaji wa maji katika halmashauri ya Biharamulo, vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.
........................BONYEZA CHINI KUSIKILIZA.......................
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment