Uzinduzi wa barabara ya Kagoma- Biharamulo hadi Lusaunga iliyogharimu shilingi bilioni 190.4 kwa mujibu wa waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof Makame Mbarawa, imezinduliwa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, leo tarehe 19/07/2017, sherehe zilizoudhuriwa na waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano, mke wa rais mama Janet Mgaufuli na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Kagera na mikoa jirani.
Katika uzinduzi huo, rais Magufuli amewataka wananchi kutumia miundombinu hiyo kwa uangalifu mkubwa, kutokana na umuhimu wake na kugharimu kiasi kikubwa cha pesa za watanzania, na kwamba serikali haitamvumilia mtu yeyote asiyelipa kodi, kwani miundombinu hiyo inatokana na kodi za wananchi hasa wanyonge.
....................BONYEZA HAPA CHINI KUSIKILIZA.................
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment