Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
ametangaza miezi mitatu ya hali ya
hatari, kwa kuwataka wananchi wake kusalia nani ya nyumba, kutokana na mapigano
ya kikabila kuongezeka nchini humo.
Msemaji wa serikali Michael Makuei,
ambaye pia ni waziri wa habari nchini humo, amesema
kuwa jeshi limepewa nguvu ya kudhibiti wapiganaji pasipokubagua nani ni nani
hasa katika jimbo la Gogrial, na kwamba haki za raia inawezekana zikawekwa kando,
ingawa rais amesisitiza wapiganaji wanajivunja.
Vyombo vya habari nchini Sudan
kusini vilisema kuwa watu kadhaa wamekwisha
uawa katika mapigano kwenye jimbo la kaskazini ya nchi, ingawa shirika la
habari la Reuters halikuweza kujitegemea kuthibitisha idadi ya watu waliouawa.
Makuei amesema hali hiyo ya hatari
pia itatumika katika maeneo jirani ya Tonj, Wau, na Aweil Mashariki, ambapo Wau ina uzoefu wa mapigano kati ya serikali na
waasi watiifu kwa aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar, wa kabila la Nuer.
Sudan
Kusini ilitumbukia katika vita vya
wenyewe kwa wenyewe tangu mwezi Desemba 2013, vikihusisha kwa kiasi kikubwa askari wa serikali na wanamgambo kutoka makabila
ya Dinka na Nuer , na kusababisha maelfu ya watu kupoteza maisha huku wengine
milioni nne kukimbia makaazi yao.
Mapigano
katika Gogrial yaliyomlazimu rais Kiir kutangaza hali ya hatari, yanatekelezwa
na wanamgambo kutoka koo za Apuk na Aguok katika
kundi la Dinka kundi linalomtii rais
Salva Kiir.
Na reuters
No comments:
Post a Comment