Kupitia kikao cha kujadili taarifa ya mkaguzi mkuu wa
serikali CAG manispaa ya Bukoba,imeibuka hoja mbalimbali ikiwemo ya baadhi ya
miradi ya maendeleo ndani ya manispaa hiyo kukwama kutekelezwa kwa muda
muafaka.
Akisoma hotuba ya mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa mkoa Kagera,mkuu wa
wilaya Bukoba Deodatus Kinawilo amesema kuwa serikali inatakiwa kupata majina ya
walioshiriki kwa aina yoyote kusababisha miradi ya maendeleo kushindwa kutekelezwa
ili wajue jinsi gani ya kushughulika nao.
Aidha amewapongeza manispaa kwa kupata hati safi kutoka kwa mkaguzi mkuu wa Serikali kufuatia jinsi
walivyotumia fedha kwa awamu hii huku akiwasihi kuendelea kukusanya mapato
ikiwa ni pamoja na kukamilisha miradi ya maendeleo iliyokwama.
Kwa upande wake meya wa manispaa ya Bukoba Chief Kalumna
amesema kuwa chanzo cha miradi mingi kukwama katika halmashauri ni kutokana na
maagizo yanayotoka ngazi za juu kutaka
halmashauri zitekelezre miradi ya
dharura nje ya bajeti.
Kufuatia hali hiyo ameiomba Serikali kuu pindi inapokuwa
inatoa maagizo izingatie miradi inayokuwa imeandaliwa na kutengewa fedha kwani
tofauti na hapo wataendelea kukwama.
…………………………………….….PICHA ZA BARAZA HILO LEO…………………………………………………..
No comments:
Post a Comment