Rais wa jamhuri wa Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Congo Kongo Joseph Kabila,
ameteua mkuu mpya wa polisi na kamanda wa polisi katika mji mkuu Kinshasa, ili
kudhibiti usalama unaondelea kuvurugika baada ya kiongozi huyo kung’ang’ania
madarakani.
Ongezeko la kubomoa magerezani,
utekaji nyara, kuongezeka kwa vurugu za wanamgambo na kufurika kwa uasi tangu
Kabila kushindwa kujiuzulu mwezi Desemba, kumeongeza hofu ya taifa la Congo
kurejea tena katika machafuko au vita.
Wafungwa elfu 4 walitoroka gerezani mwezi
mei mwaka huu katika gereza kuu mjini Kinshasa, na mpaka sasa haijulikani
wauaji wa watu wawili na kujeruhi maafisa sita wa polisi katika shambulio katika
soko kuu kuu jijini humo siku ya Ijumaa.
Rais Kabila amemteua Dieudonne Amuli
Bahigwa ambaye ni jenerali mstaafu na aliyeongoza operesheni mashariki mwa
Congo kupambana na kundi la FDLR 2009, kuchukua
nafasi ya Charles Bisengimana aliyekuwa mkuu wa polisi wa taifa la Congo.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment