MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 18 July 2017

KAGERA: VYAMA VYA USHIRIKA VYAKWAMA, SABABU ZATAJWA HAPA.

BUKOBA
Leo July 18, 2017,limezinduliwa jukwaa la wadau wa vyama vya ushirika mkoani Kagera lenye lengo la kujadili ni jinsi gani wanaweza kutatua changamoto na kuendeleza ushirika.

Kupitia jukwaa hilo zimebainishwa changamoto mbalimbali zinazosababisha vyama vya ushirika visisonge mbele,ambapo ni pamoja baadhi ya wanachama kutorejesha mikopo,elimu ndogo kwa wanachama,mitaji midogo katika baadhi ya vyama vya ushirika ikiwa ni pamoja na uhaba wa vitendea kazi kwa wakaguzi wa vyama hivyo.

Akizindua jukwaa hilo kwa niaba ya mkuu wa mkoa Kagera,mkuu wa wilaya Bukoba Deodatus Kinawilo amesema kuwa serikali inahimiza uanzishwaji wa vyama vya ushirika katika jamii,na kuongeza kuwa watumie vyama hivyo kuendeleza uchumi kwa wananchi kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya kuwaingizia kipato.

Pia ametoa rai kwa vyama vya ushirika vinavyohusika na ununuzi wa kahawa kuhakikisha wananunua mazao hayo kwa uaminifu na kutojihusisha na ubadhilifu wa aina yoyote huku akiwataka maafisa ushirika wilaya kuwachukulia hatua walanguzi wanaonunua mazao kinyume na utaratibu.

Sanjali na hayo amevipongeza vyama vya ushirika vilivyoanzisha miradi mbalimbali kutokana na kipato chao na kuwasihi wananchi kuwa wazalendo kwa kuwaunga mkono kwa vitu wanavyozalisha.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: