MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 23 July 2017

Rais atoa mwezi mmoja kwa waziri wa ujenzi.

Akihutubia wananchi wa jimbo la Kaliua, rais Magufuli amesema kuwa anataka awape raha wananchi wa Kaliua, kwamba serikali anayoisimamia, kukusanya na kutumbua pesa za wabadhilifu haiwezi kushindwa kujenga barabara.



Hatahivyo rais Magufuli amesema kuwa wananchi wote waliojenga kwenye hifadhi ya njia ya reli, wajiandae kisaikolojia kubomolewa na kupisha ujenzi wa reli mpya ya standard gauge, kuwa yeye hapendi kupindisha sheria, na kuagiza kuwa wakati wa kubomoa, waanzie na nyumba za viongozi wa CCM wanaopita na kuwadanganya watanzania kuwa wasiondoke kwenye maeneo hayo.


Amesema kuwa ameamua kutumia barabara kutoka mkoani Kagera hadi atakapofika Dar es salaam, kwa lengo la kuangalia vipande vya barabara ambavyo vimesalia bila kujengwa kwa lami, na kumwagiza waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano, kujenga barabara yenye urefu wa kilomita 28 kwa kiwango cha lami kutoka Kaliua kwenda Urambo.
................BONYEZA CHINI KUSIKILIZA...............

Na Mwanaharakati.

No comments: